BIL. 1.5 ZATUMIKA TARIME UJENZI WA SHULE ZA MSINGI NA AWALI

Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Deogratius Ndejembi amesema kiasi cha Sh Bilioni 1.512 zimepelekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara kwa ajili ya Mradi wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji  kwa Shule za  Awali na Msingi Tanzania Bara  BOOST.\n\nMhe Ndejembi ameyasema hayo leo wakati akieleza mafanikio ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwenye ziara ya Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa katika Halmashauri hiyo.\n\nMhe Ndejembi amesema Sh Bilioni 1.08 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili mpya za msingi, Sh Milioni 325 zikitolewa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 13 mapya pamoja na Sh Milioni 69 ambazo zilitolewa kwa ajili ya madarasa ya mfano elimu ya awali.\n\n“ Fedha hizo siyo kwenye elimu ya msingi tu. Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia mradi wa kuimarisha ubora wa elimu ya sekondari SEQUIP tumeleta fedha Sh Milioni 470 katika Kata ya Sirari kwenye awamu ya kwanza, awamu ya pili Sh Milioni 584 kata ya Manga na Sh Milioni 100 kwa ajili ya nyumba ya walimu Sirari,” Amesema Mhe Ndejembi.











Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"