ZAIDI YA TANI 3 ZA DAWA ZA KULEVYA ZANASWA, WATU SABA WATIWA MBARONI


NA K-VIS, BLOG, DAR ES SALAAM

MADAWA ya kulevya zaidi ya tani 3 yamekamatwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini( DCEA) katika operesheni iliyoendeshwa Dar Es Salaam na Iringa.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo amesema kiasi hicho cha dawa za kulevya kinajumuisha kilogramu 2,180.29 za dawa hatari aina ya methamphetamine na kilogramu 1001.71 aina ya heroin na kufanya kiasi kilichokamatwa kufikia kilogramu 3,182, sawa na tani 3.1.

Amesema dawa hizo zilikamatwa katika operesheni ya siku 18 kuanzia Desemba 5 hadi Desemba 23, 2023 na ilitekelezwa katika wilaya ya Kigamboni, Ubungo na Kinondoni Jijini Dar es Salaam pamoja na Wilaya ya Iringa mkoani Iringa.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema, watu saba (7) wawili kati yao wana asili ya Asia wamekamatwa kuhusiana na “mzigo” huo ambao  Mkuu huyo wa DCEA, ameuelezea kuwa ni kiasi kikubwa kuwahi kukamatwa katika historia ya nchi yetu

“ Endapo dawa hizi zingefanikiwa kuingia mtaani zingeweza kuathiri zaidi ya watu milioni 76 kwa siku, na watuhumiwa waliokamatwa ni miongoni mwa mitandao mikubwa kabisa ya wauzaji wa dawa za kulevya, inayofuatiliwa nchini na duniani.”Amefafanua.

Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, akizunhgumza jijini Dar es Salaam, Desemba 27, 2023


Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"