MAONESHO YA MADINI GEITA: NAIBU GAVANA BOT DKT. YAMUNGU KAYANDAMBILA ATEMBELEA BANDA LA PSSSF

 

Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Yamungu Kayandabila (anayezungumza pichani kulia), ametembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF), kwenye Maonesho ya 6 ya Teknolojia ya Madini, kwenye viwanja vya EPZA, Bombambili mjini Geita.

Akiwa katika banda hilo, Dkt. Kayandabila, ambaye alifuatana na Meneja Uhusuano BoT, Bi. Vicky Msina, alipokelewa na Meneja wa PSSSF,  Kanda ya Magharibi, Bw.  Geofrey Kolongo.

Bw. Kolongo alimueleza huduma zilizotolewa na PSSSF kwa wananchi na wanachama wa PSSSF ambao ni watumishi wa umma, waliotembeela banda hilo ambapo alisema, wanachama waliweza kupatiwa taarifa kuhusu uanachama wao ikiwa ni pamoja na kupata taarifa za Michango, taarifa za Mafao yatolewayo na Mfuko, wastaafu waliweza kujihakiki kwa kutumia alama za vidole lakini pia walielimishwa jinsi ya kutumia huduma ya PSSSF kiganjani, ambayo inamuwezesha mwanachama na mwajiri kupata taarifa na huduma mbalimbali za Mfuko.

Pia wanachama na wananchi walipatiwa taarifa ya uwekezaji unaotekelezwa na Mfuko, kwenye maeneo mbalimbali.

Maonesho hayo yalizinduliwa Septemba 26, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Doto Bitekoyamebeba kauli mbiu; Matumizi ya teknolojia sahihi katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi mazingira yamewaleta pamoja washiriki zaidi ya 400 na yanatarajiwa kufikia kilele Septemba 30, 2023

Dkt. Kayandabila (kushoto), akiwa na Meneja wa PSSSF, Kanda ya Magharibi, Bw. Godfrey Kolongo wakati akisaini kitabu cha wageni
Mkuu wa Wilaya ya Chunya,  mkoani Mbeya, Mhe. Simo Mayeka, (kushoto), akipokea muongozo wa Wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF), kutoka kwa Bw. Nathan Makuchilo, Afisa Mafao Mwandamizi wa Geita







 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"