PSSSF KUWEKEZA ZAIDI KWENYE TEHAMA, RASILIMALI WATU ILI KUONEGZA UBORA WA UTOAJI HUDUMA

 

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, DAR ES SALAAM

KATIKA kuhakikisha Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unaendelea kutoa huduma bora kwa wanachama wake, sasa unaelekeza nguvu zake katika matumizi ya TEHAMA na kuendeleza rasilimali watu ili kuongeza ubunifu na ufanisi, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, amesema.

CPA. Kashimba ameyasema hayo kwenye kikao kazi baina ya Mfuko, Ofisi ya Msajili wa Hazina (TR) na Wahariri wa vyombo vya habari, wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mfuko tangu kuanzishwa kwake Agosti, 2018 hadi Agosti, 2023, kwenye Makao Makuu ndogo ya PSSSF, jengo la Golden Jubilee Tower, jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2023,

“Kama kuna namna ya kuufanya Mfuko uwe wa kisasa zaidi basi hayo ndiyo matamanio yetu na tumeanza, lengo ni kuifanya taasisi iwe rafiki zaidi kwa wanachama wake na yenye miundombinu ya kutoa huduma bora zaidi bila ya usumbufu wowote.” Alisema.

Alisema kwa sasa Mfuko unatumia TEHAMA kwa zaidi ya asilimia 90 katika kazi zake zote na inategemea kufika asilimia 100 ifikapo Juni, 2024;

“Mifumo hii ni matokeo ya uwekezaji na uvumbuzi wa Mfuko katika Mifumo kwa kutumia wataalamu wetu wa ndani ili kuboresha huduma kwa wateja na pia kuimarisha usalama katika kutunza nyaraka, kufanya malipo na kupokea malipo mbalimbali na matumizi mengine.” Alifafanua CPA. Kashimba

Alisema kupitia maboresho yaliyofanywa na Mfuko, Mwajiri anaweza kutengeneza ankara na kulipa michango moja kwa moja akiwa ofisini kwake bila kuhitaji msaada wa mtu.

“Wanachama pia wanaweza kupata taarifa zao kupitia simu za kiganjani, wastaafu na wategemezi wanaweza kujihakiki kwa kutumia alama za vidole (biometric) na tumeenda mbali zaidi, hata mwanachama akiwa nyumbani kwake anaweza kutumia simu janja (smart phone) kupitia App ya PSSSF kiganjani na akajihakiki.” Alifafanua.

Kuhusu hali ya Mfuko, CPA Kashimba aliwaambia Wahariri kuwa, thamani ya Mfuko wa PSSSF, imefikia shilingi trilioni 8.07 katika kipindi cha miaka mitano tangu kuanzishwa kwake huku thamani ya uwekezaji ikifikia kiasi cha shilingi  trilioni 7.92.

Akifafanua kuhsuu uwekezaji alisema unahusisha Hati fungani za Serikali (60% chini ya kikomo cha 100%), Uwekezaji katika Majengo (15% chini ya kikomo cha 30%; kiwango cha upangishaji huu ni 100% kwa majengo ya makazi na 72% kwa majengo ya kupangisha kwa ajili ya ofisi huku matarajioni yakiwa ni kufika asilimia 80% mwishoni mwa mwaka huu wa fedha.

Maeneo mengine ya uwekezaji ni Hisa za Makampuni (12% chini ya kikomo cha 20%), Amana za Mabenki (7% chini ya kikomo cha 35%); na Maeneo mengine (6%).

Aidha, kuhusu uandikishaji Wanachama na ulipaji wa Mafao alisema hadi kufikia Juni 2023, idadi ya wanachama wa PSSSF ni 731,183 na umetumia kiasi cha shiling trilioni 8.88 kulipa mafao kwa wanufaika 262,095, huku ukilipa pensheni ya kila mwezi shilingi bilioni 67 kwa wanufaika 164,828 na pensheni hulipwa tarehe 25 ya mwezi husika bila kuchelewa na sasa Mfuko unalipa Mafao ndani ya siku 60 kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, (TEF), Bw. Deodatus Balile, aliwashukuru waandaaji wa kikao hicho kwani kimetoa fursa kwa Wahariri kujifunza mengi kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Mfuko.

Vyombo vya habari ndio njia pekee ya kuwafikia wananchi kwa uhalisia.” Alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari Agosti 31, 2023
Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mfuko tangu ulipoanzishwa hadi Agosti 2023.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, (TEF), Bw. Deodatus Balile, akizungumza kwenye kikao hicho.
Meneja PSSSF, Kanda ya Ilala, Bi. Uphoo Swai (kushoto), Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, Bw. James Mlowe (katikati) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikali, Ofisi ya Msajili wa Hazina (TR), Bw. Eric mkuti, wakifuatilia wasilisho la Mkurugenzi Mkuu PSSSF, CPA. Hosea Kashimba.
Mhariri Mstaafu wa gazeti la Uhuru, Joe Nakajumo, akipitia kijitabu cha PSSSF cha Muongozo wa Mwanachama Namba 3
Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu PSSSF, CPA. Hosea Kashimba (wapili kulia), Mwenyekiti wa TEF, Bw. Deodatus Balile (wakwanza kulia), Meneje Uhusiano na Elimu kwa Wanachama PSSSF, Bw. James Mlowe (wakwanza kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Msajili wa Hazina (TR), Bw. Eric Mkuti.
Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mfuko tangu ulipoanzishwa hadi Agosti 2023.
Mtendaji Mkuu wa Mtandao wa Fullshangwe Blog, Bw. John Bukuku
Mhariri wa gazeti la Jamhuri, Bw. Manyerere Jackton 
Mhariri Mkuu, ETV na EFM, Bi. Scholastica Mazula.
Bi. Kisa Mwaipyana kutoka Channel Ten
Baadhi ya Wahariri waliohudhuria kikao hicho.
CPA. Hosea Kashimba (kulia) akiongozana na Bw. Deo Balile (katikati) na Bw. James Mlowe, mwishoni mwa kikao hicho.
Afisa Uhusiano Mkuu, PSSSF, Bw. Abdul Njaidi (kulia) akibadilishana mawazo na Mhariri  wa gazeti la Jamhuri Bw. Manyerere Jackton.
Mhariri Mkuu, gazeti la The Guardian, Bw. Wallace Maugo (kushoto), akizungumza jambo na aliyewahi kuwa Magazeti ya Chama Cha Mapinduzi ya Uhuru na Mzalendo, Joe Nakajumo,
Watumishi wa PSSSF kutoka kulia, Bi. Hidaya Mganga, Bi. Fatma Alhady na Bi.Coleta Mnyamani. 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"