MKOA WA PWANI WAONGOZA UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE KITAIFA
NA MWANDISHI WETU, PWANI
MKOA
wa Pwani umetunukiwa tuzo baada ya kuibuka kinara katika utekelezaji wa Mkataba
wa Lishe kwa mwaka 2022/23.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Angela Kairuki ndiye aliyemkabidhi tuzo
hiyo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Alhaji SAboubakar Kunenge.
Taarifa
zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa - (OR -
TAMISEMI) zimeeleza kuwa Mkoa huo umefuatiwa na Lindi katika nafasi ya pili
huku nafasi ya tatu ikienda kwa mkoa wa Iringa.
Kwa
upande wa nafasi za Halmashauri, Mkoa wa Pwani umefanikiwa kuingiza halmashauri
za Kibaha TC na Kibaha DC katika nafasi kumi za mwanzo.
Kibaha
TC imekuwa ya na Kibaha DC ikiwa ni ya 10 huku hamashauri zingine za mkoa huo
zikiwa zimeshika nafasi juu ya 100 za mwanzo.
Halamshauri
hizo na nafasi zao kitaifa kwenye mabano ni Kisarawe (17), Rufiji (25), Bagamoyo
(26) na Kibiti (54). Zingine ni Chalinze (59), Mafia (91) na Mkuranga (93).
Comments
Post a Comment