RC CHALAMILA ATOA WIKI MOJA KWA WAFANYABIASHARA MWENGE WALIOTELEKEZA VIBANDA KURUDI MARA MOJA.

Ni kufuatia wafanyabiashara hao kuondoka eneo walilopangwa na kuhamishia biashara Barabarani.

 Amuelekeza Mkandarasi anaejenga Majengo ya kituo Cha Afya Kinondoni kuzingatia ubora.

Apongeza Halmashauri ya Kinondoni kwa kubuni mradi wa Stendi ya Mwenge na Uwanja wa Mpira.

Ampongeza Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kutoa bilioni 1.5 kwaajili ya Maboresho ya Elimu program ya Boost.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe, Albert Chalamila ametoa muda wa wiki Moja kwa Wafanyabiashara wa Soko la Mwenge Coca cola walioacha vibanda vyao na kurudi kupanga biashara Barabarani kurudi kwenye eneo walilopangwa mara Moja.

RC Chalamila ametoa maelekezo hayo wakati wa Ziara ya kukagua Miradi mbalimbali ya Maendeleo Wilaya ya Kinondoni

Akikagua mradi wa ujenzi wa Kituo Cha Mabasi Mwenge RC Chalamila amepokea malalamiko ya Wafanyabiashara waliosema kitendo Cha wafanyabiashara kupanga bidhaa chini imepekea kukosekana kwa wateja na kusababisha mitaji ya biashara kufa.

Kutokana na Hilo RC Chalamila ameelekeza Jeshi la polisi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Kinondoni kuratibu zoezi la kuhakikisha wafanyabiashara wanarudi kwenye eneo walilopangwa.

Aidha RC Chalamila ameipongeza Halmashauri ya Kinondoni kwa kubuni mradi wa Stendi ya Mabasi Mwenge na Ujenzi wa Uwanja wa Mpira kwaajili ya timu ya KMC kwakuwa kukamilika kwake Itasaidia ongezeko la Mapato kwa Halmashauri.

Ili kuhakikisha uwekezaji huo unakuwa na tija RC Chalamila ameelekeza Halmashauri hiyo kuzingatia uwazi kwenye mchakato mzima wa utoaji wa frem za maduka, uwiano mzuri wa gharama ya kupanga ambapo pia ameshauri maduka ya jumla kuwekwa kwenye gorofa za juu na wale wafanyabiashara za rejareja kupangwa maduka ya chini.

Pamoja na hayo RC Chalamila ametembelea ujenzi wa jengo la gorofa Moja kwenye kituo Cha Afya Kinondoni ambapo panajengwa jengo la Wazazi, jengo la upasuaji na jengo la kulaza wagonjwa wa nje ambapo amemuelekeza Mkandarasi kutoka kampuni ya Gemini Engineering Construction ltd kuhakikisha ujenzi unazingatia ubora kwa mujibu wa mkataba.

Hata hivyo RC Chalamila ametembelea na kuzindua ujenzi wa miundombinu kwenye shule ya msingi Kundichi ambapo amempongeza Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Shilingi bilioni 1.5 kupitia programu ya Boost inayolenga kuboresha mazingira ya elimu ambapo miongoni mwa shule zilizonufaika ni shule ya msingi Kundichi, Kisauke, Mapinduzi, Mchangani, Mkwawa, Mtambani a Shule ya Ali Hassan Mwinyi.





 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"