“SERIKALI KUJENGA VITUO MAALUM VYA UREKEBU” WAZIRI MHAGAMA
Na Mwandishi Wetu – Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge
na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama, amesema Serikali imejenga vituo maalum
vya urekebu na ufundi stadi ili kuwasadia vijana na wale wote
wanaoathirika baada ya kutumia dawa za kulevya.
Ameyasema hayo mapema leo Mei 30 2023, Bungeni Dodoma
wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu hali ya dawa za
kulevya ya mwaka 2022 ambapo amessema kwa mujibu wa utafiti unaonyesha
uwepo wa kiwango kikubwa cha uzalishwaji na ulimaji wa bangi.
Waziri Mhagama alisema, kwa mwaka ujao wa fedha
2023/2024 Serikali imetenga bajeti ya shilingi Bilioni nane nukta saba (Bilioni
8.7) zitakazotumika kujenga vituo vya urekebu na ufundi stadi,
vitakavyosaidia kubadilisha tabia za vijana wanaotumia dawa za kulevya,
“Vituo hivyo vitakuwa na kazi kubwa ya kuwaondoa kwenye matumizi
ya dawa na kuwapa shunguli nyingine watakazotakiwa kuzifanya zitakazotokana na
shughuli za ujuzi, ambazo watafundishwa kwenye vitu hivyo.” Alifafanua.
Aliendelea kusema kuwa, kupitia Wizara ya Kilimo, Serikali
itafanya utafiti, ili maeneo yanayolima bangi kibiashara kama vile Kisimiri Juu
mkoani Arusha, kusaidiwa kulima mazao mbadala na juhudi za Serikali za
kukomesha kilimo hicho zinaweza kuwasaidia kutoka kwenye biashara hiyo haramu kwa
makusudi ya kuongeza kipato, na kuwafanya vijana na watumiaji kuwa salama.
“Kwa Jiji la Dodoma pekee tunategemea kutumia kiasi cha shilingi
Bilioni mbili, kujenga kituo hicho katika Eneo la Itega.” Alisema.
Awali akiongea katika mkutano huo na waandishi wa habari
aliitaja baadhi ya mikoa inayoongoza kwa kulima bangi nchini kuwa ni
pamoja na Arusha, Manyara, Mara na Njombe,na kuitaja baadhi ya Mikoa
itakayojengwa vituo hivyo kuwa ni pamoja na Shinyanga, Kilimanjaro,
Mwanza na Arusha.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama akitoa Taarifa kuhusu hali ya dawa za kulevya ya mwaka 2022 kwa waandishi wa habari tarehe 30 Mei, 2023 Jijini Dodoma.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa ya hali ya dawa za kulevya ya mwaka 2022 aliyoitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama alipokutana nao leo Mei 30, 2023.
Comments
Post a Comment