MKURUGENZI MKUU WA WCF AKUTANA NA WANUFAIKA WA FIDIA

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma (katikati) akisalimiana na Wanufaika wa Fidia inayotolewa na WCF, Bw. Deus Anthony (kulia) na Bw. Ramadhan Juma kwenye kilele cha siku ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi katika viwanja vya Tumbaku mjini Morogoro Aprili 28, 2023.

Wawili hao wamepata ulemavu wa kudumu baada ya kuumia kwa nyakati tofauti wakati wakitekeleza majukumu ya waajiri wao.

Wakati Bw. Deus Anthony ambaye aliumia wakati akishiriki ujenzi wa barabara kati ya Iringa-Igawa alikatika mguu na kufaidika na fao la matibabu kutoka WCF hadi alipopona.

“Nilikatika mguu   wa kushoto wakati nikiwa kazini mwaka 2017, WCF wamekuwa na mimi katika matibabu hadi kupona na kasha kunipa mguu w abandia, naweza kutembea bila ya shida yoyote.” Amefafanua , Bw. Anthony.

“Nawashukuru WCF kwa kuniwezesha kuyamudu maisha, pensheni ninayolipwa kila mwezi kutokana na ulemavu wangu wa kudumu,  nimekuwa nikidunduliza na hatimaye nimefanikiwa kumiliki bajaji yangu mwenyewe kutokana na kipato hicho cha kila mwezi.” Alisema na kuongeza…. hivi sasa nafikiria kukodi shamba ili nilime maaharage huko Mikumi.” Amesema

Mnufaika mwingine ni Bw. Ramadhan Juma, mfanyakazi kwenye kiwanda kimoja mjini Kibaha, mkoa wa Pwani.

Yeye alikatika mkono wakati akiwa kwenye eneo lake la kazi, na ameelezea jinsi WCF ilivyomuhudumia tangu anauguza mkono wake hadi kupona.

“Nilikatika mkono wakati naendesha mashine pale kiwandani, nimetibiwa na kupona na kama haitoshi nikapatiwa mkono wa bandia na WCF.” Alisema mnufaika huyo.

Alisema fidia kila mwezi anayolipwa ba WCF imekuwa ikimsaidia katika kuhudumia wazazi wake lakini pia wadogo zake.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma (katikati) akisalimiana na Wanufaika wa Fidia inayotolewa na WCF, Bw. Deus Anthony (kulia) na Bw. Ramadhan Juma kwenye kilele cha siku ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi katika viwanja vya Tumbaku mjini Morogoro Aprili 28, 2023.
Mkurugenzi Mkuu WCF, Dkt. John Mduma (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar.
Dkt. Mduma akikaribishwa na Meneja wa PSSSF Kanda ya Mashariki, Bi. Zaida Mahavu na Afisa Uhusiano Mkuu Bw. Abdul Njaidi kwenye banda la PSSSF.
Mkurugenzi Mkuu WCF, Dkt. John Mduma (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini, Dkt. Abdulsalaam Omar alipotembeela banda la NSSF
Mkurugenzi Mkuu WCF, Dkt. John Mduma akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa WCF mbele ya banda la Mfuko huo baada ya kutwaa tuzo

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"