WAZIRI TABIA MAULID MWITA AWATAKA MAAFISA HABARI SERIKALINI KUHUWISHA TAARIFA KWENYE TOVUTI NA MITANDAO YA KIJAMII YA SERIKALI

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Tabia Maulid Mwita amefunga Kikao Kazi cha 18 cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Serikalini (TAGCO) na kuwataka kuhuwisha taarifa zilizomo kwenye tovuti na mitandao ya kijamii ya Serikali.

Ameyasema hayo Machi 30, 2023 mbele ya washiriki kutoka Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Darves Salaam .

“Niwangapi kati yenu ambao mmetekeleza agizo la Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye aliyewataka kuhakikisha taarifa za serikali zinawekwa mara kwa mara kwenye tovuti na mitandao ya kijamii ili kuwa na ufanisi katika kutumia njia za kisasa za mawasilino katika utoaji taarifa kwa umma?.” Aliuliza.

Alisema anaungana na Mhe. Nape ambaye alisema baadhi ya tovuti na mitandao hiyo ya serikali ina taarifa za muda mrefu zilizopitwa na wakati.

“Tuna kazi kubwa mbele yetu ya kufanya nawasihi mnapotoka hapa muende kutumia elimu mliyopata ili kupeleka mabadiliko kwa kuondoa taarifa hizo za muda mrefu na kuweka taarifa mpya ambazo ziko nyingi na zina tija.”Alisisitiza Mhe. Mwita.

Alisema ulimwengu wa sasa unakwenda na mitandao ya kijamii inayofatiliwa na wananchi wengi.

Alisema Maafisa hao wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha Serikali inatoa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Toeni taarifa hususan takwimu za miradi, fedha zilizotumika, manufaa ya miradi husika kwa maendeleo ya wananchi na wajibu wa wananchi katika miradi husika.” Alibainisha.

Akimkaribisha Waziri Mwita, Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Kundo Mathew alisema madhumuni ya kikao yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupitia ushirikiano wa Wizara, Idara ya Habari Maelezo na TAGCO.

Alisema Kikao Kazi cha 18 kilishirikisha Maafisa Habari kutoka Wizara zote, Idara na Taasisi za Umma na Serikali Kuu, TAMISEMI na Sekretarieti za Mikoa.

Alisema Wizara inaelewa umuhimu wa Maafisa Habari, Mawasiliano serikalini ambao ni daraja la mawasiliano ya Serikali na wananchi wake.

Jukumu la msingi la Maafisa hao ni kuisemea serikali kwa kutoa taarifa sahihi kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo, miradi ya kimkakati na kujenga mawasiliano chanya na vyombo vya habari, wananchi na taasisi binafsi, alisema Mhandisi Kundo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde kwa niaba ya wanachama wa Chama hicho amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali yake ya Awamu ya Sita kwa kutatua changamoto ya muda mrefu ya muundo wa vitengo vya Habari, Mawasiliano na Uhusiano vya Serikali.

Amesema jambo hilo  limeinua morali na nguvu ya kufanya kazi kwa bidii katika kuisemea na kuiunganisha Serikali na wananchi.  "Jambo lingine la kumshukuru Mhe. Rais na Serikali yake kwa ujumla ni nia yake thabiti ya kutaka na kuelekeza maafisa wake wa habari tutumike ipasavyo katika kutekeleza majukumu yetu katika Wizara na Taasisi za Umma, jambo hili linatupa nguvu ya kusimamia na kutekeleza majukumu yetu ya kihabari.” Alisisitia Bi. Sarah Kibonde. 

Washiriki wa Kikao hicho watakamilisha siku ya tano ya mafunzo kwa kufanya ziara ya kutembelea Bandari ya Dar es Salaam na Mradi wa Kimkakati wa ujenzi wa reli ya Kisasa SGR Ijumaa Machi 31, 2023.

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Tabia Maulid Mwita akitoa hotuba ya kufunga Kikao Kazi cha 18 cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Serikalini (TAGCO) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam Machi 30, 2023. 
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Tabia Maulid Mwita akitoa hotuba ya kufunga Kikao Kazi cha 18 cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Serikalini (TAGCO) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam Machi 30, 2023. 
Wajumbe wa Kikao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri
Wajumbe wa Kikao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri
Wajumbe wa Kikao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri
Wajumbe wa Kikao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri
Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Kundo Mathew, akizungumza kwenye Kikao hicho.
Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Kundo Mathew, akizungumza kwenye Kikao hicho
Kaimu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maafisa Habari Zanzibar (ZICOO), Bi. Raya Hamad Suleiman (wapili kushoto) na baadhi ya wajumbe wa Jumuiya hiyo wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi
Katibu Mkuu wa TAGCO, Bw. Abdul Njaidi
Wajumbe wa Kikao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri


Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa.
Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde akielekea mahala pa kutolea hotuba yake.
Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde, akitoa hotuba yake.
Kaimu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maafisa Habari Zanzibar (ZICOO), Bi. Raya Hamad Suleiman, akitoa neno la shukrani.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Selestine Kakele (katikati) akikabidhiwa shati la TAGCO na Mwenyekiti Bi. Sara Kibonde na Katibu Mkuu Bw. Abdul Njaidi. Kwa takriban siku nne za Kikao hicho Bw. Kakele  amekuwa akisimamia kikao hicho kama Mwenyekiti.

Wajumbe wa Kamati Tendaji ya TAGCO wakungana na washiriki kupongeza hotuba ya mgeni rasmi.

Msemaji wa Jeshi la Polisi Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP), David Misiime na washiriki wengine wakionyesha furaha mwishoni mwa Kikao hicho.

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"