VYOMBO VYA HABARI VINA MCHANGO MKUBWA KATIKA SEKTA YA UCHUMI NA FEDHA-NAIBU GAVANA BoT JULIAN BANZI

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), anayeshughulikia Utawala na Udhibiti wa Ndani,  Bw. Julian Banzi amesema vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kuelimisha umma kuhusu masuala ya Uchumi na Fedha.

Akizungumza kwa niaba ya Gavana wa Benki Kuu wakati akifungua Semina ya siku moja ya masuala ya Uchumi na Fedha, kwa wahariri wa vyombo vya habari kwenye Makao Makuu ndogo ya BoT jijini Dar es Salaam leo Februari 27, 2023, Bw. Banzi alisema,  BoT ina amini kuwa wahariri na waandishi wa habari wakiwa na uelewa wa kutosha kuhusu masuala ya Fedha na Uchumi, watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kufikisha ujumbe ulio sahihi na kwa lugha rahisi kwa wananchi.

Alisema,  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria inayoipa BoT mamlaka ya  kusimamia Sekya ya Huduma Ndogoz a Fedha.

Chini ya Sheria hiyo BoT ndiyo inayosajili, Kusimamia na Kudhibiti biashara ya huduma ndogo za Fedha Tanzania Bara. 

"Hapo nyuma kulikuwa na changamoto kidogo kwa Taasisi za huduma ndogo za fedha kama vile zinazotoa mikopo midogo midogo, vikoba hivyo Bunge lilitunga sheria ili kuondoa changamoto hizo.. Ni vizuri mkapata nafasi ya kuelezwa kuhusu sekta hiyo ndogo ya fedha na changamoto zilizokuwepo  ambazo zilikuwa zinawaumiza wakopaji.” Alifafanua.

Alisema BoT inashirikiana na vyombo vya habari kwa nia ya kufikisha ujumbe kwa wananchi ili waweze kuelewa fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye sekta ya fedha na hivyo kufaidika nazo.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bw. Bakari Machumu aliishukuru BoT kwa kuandaa mafunzo hayo kwa wahariri kwani yatasaidia sana katika kuongeza uelewa kuhusu masuala ya Uchumi na Fedha. Kuu.

NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Julian Banzi (kushoto), akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari nchini kwenye semina ya siku moja ya masuala ya Uchumi na Fedha iliyofanyika kwenye ukumbi wa Makao Makuu ndogo ya BoT jijini Dar es Salaam Februari 27, 2023. Kulia ni Meneja Msaidizi wa Uhusiano na Itifaki BoT, Bi. Noves Moses.
NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Julian Banzi
NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Julian Banzi.
Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bw. Bakari Machumu
NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), anayeshughulikia Utawala na Udhibiti wa Ndani,  Bw. Julian Banzi (kulia), akijadiliana jambo na Afisa Uhusiano Mkuu Mwandamizi Idara ya Uhusiano na Itifaki, Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Lwaga Mwambande. 


Meneja Msaidizi wa Idara ya Uhusiano na Itifaki BoT, Bi. Noves Moses, akizungumza
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Gavana wa BoT, Bw. Banzi Banzi.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Gavana wa BoT, Bw. Banzi Banzi.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Gavana wa BoT, Bw. Banzi Banzi.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Gavana wa BoT, Bw. Banzi Banzi.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Gavana wa BoT, Bw. Banzi Banzi.
NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), anayeshughulikia Utawala na Udhibiti wa Ndani,  Bw. Julian Banzi(kulia) akiagana na Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Bw. Bakari Machumu baada ya ufunguzi wa semina. Kushoto ni Meneja Msaidizi wa Uhusiano na Itifaki BoT, Bi. Noves Moses.
Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano na Itifaki Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bi. Noves Moses (kulia), akisalimiana na Mhariri Bw. Bakari Kimwanga.

Picha ya pamoja.

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"