RAIS SAMIA AMLILIA PAPA MSTAAFU BENEDICT XVI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesikitishwa na taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu Mstaafu Benedict XVI.
Katika salamu sale fupu alizozitoa kupitia mitandao ya kijamii, Dkt. Samia ameandika,
"Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu Mstaafu Benedict XVI, ambaye alijitoa maisha yake kutumikia wengine. Natuma salamu za pole kwa Baba Mtakatifu Francisko, waumini wa Kanisa Katoliki Tanzania na Duniani kote. Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi. Amina."
Comments
Post a Comment