KAMATI YARIDHIA HATUA ZINAZOCHUKULIWA NA BoT KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA YA FEDHA

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

KAMATI ya Sera ya Fedha (Monetary Policy Committee) imeridhia  Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iendelee na utekelezaji wa sera ya fedha inayolenga kupunguza ongezeko la ukwasi katika uchumi kwa mwezi Novemba na Desemba 2022.

Tamko hilo la Kamati limetolewa kufuatia kikao chake cha Novemba 28, 2022 ambapo ilifanya tathmini ya utekelezaji wa sera ya fedha na mwenendo wa uchumi na kwa kuzingatia athari za mtikisiko wa uchumi

duniani kwenye mfumuko wa bei na shughuli za uchumi.

Kwa mujibu wa Taarifa ya Brnki Kuu iliyotolewa kwa vyombo vya Habari Novemba 29, 2022 imesema utekelezaji huu wa sera ya fedha unalenga kuhakikisha kuwa mfumuko wa bei unaendelea kubakia ndani ya lengo na kuwezesha ukuaji wa uchumi nchini.

Taarifa kamili inapatikana hapo chini.

Gavana wa Benki Kuu, Prof. Florens Luoga (Picha ya Maktaba)



Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"