TANZANIA TUKO MILIONI 61.7; RAIS SAMIA

Kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu Sura 351 ya 2015, na kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2025 Ibara 206, na kwa Mamlaka niliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ninawatangazia rasmi kuwa Tanzania ina idadi ya watu wapatao 61,741,120.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akinyanyua Kitabu cha Muongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 katika sherehe zilizofanyika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma tarehe 31 Oktoba, 2022.
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi Vitabu vya Matokeo ya Mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 pamoja na Kitabu cha Muongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua Kitabu cha Muongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 katika sherehe zilizofanyika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma tarehe 31 Oktoba, 2022. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akibonyeza Kitufe kuzindua Matokeo ya Mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi katika Sherehe zilizofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma tarehe 31 Oktoba, 2022. 



*Wanawake ni wengi kuliko wanaume

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema idadi ya Watu nchini imefikia Milioini 61,741,120. 

Rais ametangaza hayo Oktoba 31, 2022 katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma wakati akitoa matokeo ya mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi iliyofanyika Nchi nzima Agosti 23, 2022.

Mhe. Rais Samia amesema matokeo hayo yanaifanya Tanzania bara kuwa na Idadi ya Watu Milioni 59,851,357,  wakati Zanzibar ina watu Milioni 1,889,773.

Matokeo hayo yanaonyesha Wanawake ni wengi kuliko wanaume na wanafanya idadi yao kuwa Milioni 31,687,990 sawa na asilimia 51% huku Wanaume wakiwa Milioni 30,053,130 sawa na asilimia 49%.

Aidha kwa upande wa majengo, Tanzania kuna jumla ya Majengo Milioni 14,348,373. Tanzania Bara Ina majengo Milioni 13,907,951, huku Tanzania Zanzibar Kuna majengo Milioni 440,420.

Sensa ya Watu na Makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10 ambapo Sensa ya mwisho kufanyika nchini ni ile ya mwaka 2012 ambapo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa na idadi ya watu Milioni 44,929,002.

Hivyo Sensa ya mwaka 2022 ilikuwa ni sensa ya Sita (6) kufanyika nchini baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002 na 2012.

Umuhimu wa kipekee wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni pamoja na pamoja na kuisadia Serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidia mchakato wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025, mageuzi ya masuala ya afya na jamii, pamoja na ufuatiliaji wa ajenda za maendeleo za kimataifa;

Taarifa za idadi ya watu husaidia katika mamlaka za wilaya katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ambayo huakisi matakwa ya watu katika ngazi husika na kusaidia kwenye uwiano wa mgawanyo wa rasilimali.

Taarifa za msingi za hali ya kidemografia, kijamii na kiuchumi za idadi ya watu na makazi za mipango katika ngazi zote;

Kigawio katika kukokotoa viashiria vingine mfano Pato la mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa, Ajira na ukosefu wa Ajira na kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi;

Taarifa itakayowezesha serikali kujua ongezeko la idadi ya watu, kwa mgawanyo na viashiria vingine, ambavyo ni muhimu kwa usimamizi wa mazingira na Msingi wa utawala bora na ujumuishaji wa demokrasia.




Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"