MCHUNGAJI PETER MSIGWA "AMWAGIA SIFA" RAIS SAMIA, NI KUTOKANA NA FILAMU YA THE ROYAL TOUR
NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
MJUMBE
wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Mchungaji Peter Msigwa amempongeza Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kufuatia juhudi kubwa
anazofanya za kuitangaza nchi kupitia filamu ya The Royal Tour.
Mchungaji
Msigwa ameita kitendo hicho cha Mhe. Rais kuwa ni jambo la kizalendo na
anapaswa kutiwa moyo na kila Mtanzania.
Akiandika
kwenye ukurasa wake wa tweeter Mchungaji Msigwa ameendelea kusema kuwa Kwa
namna iwayo yote ile hii ni hatua kubwa positive.
“Inawezekana
kunaweza kuwa na mapungufu kwenye Filamu ya ROYAL TOUR! Lakini jambo
alilolifanya Mh SSH ni jambo la kizalendo na la kutiwa moyo. Mara nyingi nikiwa
bungeni nimeshauri kuitangaza Tanzania kwa nguvu kimataifa. Kwa namna iwayo
yote ile hii ni hatua kubwa positive.” Ameandika Mchungaji Msigwa.
Tayari
filamu ya The Royal Tour imeshazinduliwa nchini Marekani na sasa inaendelea
kufanyiwa uzinduzi nchini ambapo Aprili 28, 2022 ilizinduliwa kwenye mji wa
kitalii wa Arusha, na kasha itafuatiwa na miji ya Dar es Salaam na Zanzibar
lengo kubwa la filamu hiyo ni kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana
nchini ambapo Rais ndiye muhusika mkuu kwenye filamu hiyo na amecheza kama Tour
Guide
Rais Samia
Mchungaji Peter Msigwa
Comments
Post a Comment