BOTI YAZAMA PEMBA, MIILI 9 YAOPOLEWA, 15 WANUSURIKA NA WENGINE BADO HAWAJULIKANI WALIPO
Na MWANDISHI wetu.
WATU Tisa
(9) wamefariki baada ya boti waliokuwa wakisafiria kuzama baharini kisiwani Pemba,
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Pemba, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Richard
Tadei amethibitisha.
ACP Tadei
amesema boti hiyo iliyokuwa na abiria zaidi ya 30 ilikuwa ikisafiri
kutoka Chakechake kuelekea kisiwa kidogo cha Panza kilichoko mkoa wa Kusini Pemba
Januari 4, 2022.
"Watu hawa walikuwa wanaelekea msibani na katika hatua ya awali ya uokoaji tumefanikiwa kupata miili 9, na watu 15 wakiwa hai". Alisema ACP Tadei.
Hata hivyo hakuaema chanzo Cha ajali hiyo ni nini hasa.
Alisema Kazi ya uokoaji iliyokuwa ikiongozwa na vyombo vya ulinzi na Usalama kwa kushirikiana na wananchi imeahirishwa kwa muda kutokana na hali mbaya ya hewa na inatarajiwa kuendelea tena leo.
Alisema Miili ya waliofariki imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Mkoani ya Abdallah Mzee kwa ajli ya uchunguzi wa kitabibu na baada ya hapo wananchi wataruhusiwa kutambua wapendwa wao kwa ajili ya mazishi.
ina lilah wainailaih rajiun
ReplyDelete