PSSSF YATWAA TUZO YA UMAHIRI UWASILISHAJI BORA WA TAARIFA ZA MAHESABU 2020
MFUKO
wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetwaa Tuzo ya Umahiri katika
Uwasilishaji wa Taarifa za mahesabu kwa
mwaka 2020.
Akizungumza
baada ya kupokea Tuzo hiyo katika hafla ya kufunga mafunzo pamoja na utoaji wa
Tuzo za umahiri katika uandaaji wa Taarifa za Fedha ya Mwaka 2020 (Best
Presented Financial Statements for the Year 2020 Awards) kwa Taasisi, Makampuni
pamoja na Mashirika zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa
Hesabu Tanzania (NBAA) zilizofanyika katika hotel ya APC Bunju jijini Dar es
Salaam Desemba 3, 2021, Mkurugenzi wa Fedha, PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi alisema
Ushindi huo ni ishara ya kwamba PSSSF inaandaa mahesabu kwa kuzingatia vigezo
vilivyowekwa kimataifa lakini pia inaashiria uwepo wa weledi wa tasnia husika
kwa upande wa watumishi.
“Sambamba
na hayo niliyoyasema pia inaashiria uwepo wa usimamizi makini wa fedha za
wanchama na hii inatupatia heshima kama
taasisi.” Alisema Mkurugenzi huyo wa Fedha PSSSF.
Aliwahakikishia
Wanachama dhamira ya PSSSF kuhakikisha
usalama wa michango yao unazingatiwa kwa kiwango cha juu wakati wote, ikiwa ni
pamoja na kuwepo uwazi kwenye usimamizi na utunzaji wa rasilimali za Mfuko.
We are proud of you daughters of our land. God bless !
ReplyDelete