WEKEZENI KWENYE MIRADI AMBAYO HAITAWASUMBUA; MKURUGENZI MKUU PSSSF, CPA HOSEA KASHIMBA

 NA MWANDISHI WETU

MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), CPA. Hosea Kashimba amewaasa wastaafu watarajiwa kuwekeza kwenye miradi ambayo haitawasumbua pindi watakapokuwa nje ya utumishi wa Umma.

CPA. Kashimba ametoa rai hiyo leo Agosti 5, 2021, wakati akifunga mafunzo ya Awamu ya Kwanza ya Semina kwa wastaafu watarajiwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 jijini Dar es Salaam.

“Tunawaomba sana muwekeze katika mambo ambayo hayatawasumbua kama mlivyofundishwa katika semina hii…mfannye vitu ambavyo mnavifahamu.”Alisema.

Alitoa mfano wa Mstaafu mmoja ambaye yeye baada ya kulipwa mafao yake alienda kununua daladala 10 ili afanye biashara ya usafirishaji na kwakuwa hakuwa na uzoefu wowote wa biashara hiyo haikudumu na biashara hiyo “ikafa”.

“ Kwa hiyo tuangalie kama ni kuanza biashara za daladala ni vema ukaanza mapema ukiwa bado uko kwenye utumishi na usisubiri kustaafu halafu ndiyo uanze biashara ya daladala, itakusumbua sana,”alisema.

Alisema ni matumaini yake semina hiyo imewasaidia sana wastaafu hao kujua namna gani wanapaswa kuishi wakiwa nje ya utumishi wa umma na kuwaandaa kufanya matumizi sahihi ya fedha watakazolipwa ili waendelee kuishi maisha ya furaha na amani.

Washiriki wa semina hiyo iliyowaleta pamoja watumishi wa umma wa kada mbalimbali jijini Dar es Salaam ambao wanatarajia kustaafu katika vipindi tofauti ambapo wapo waliobakiza miaka mitano wastaafu, wengine mitatu, miwili na mmoja.

Katika awamu hii ya kwanza semina hizo zimeshafanyika kwenye mikoa mbalimbali zikianza Julai 14, 2021 jijini Dodoma, na kuendelea kwenye mikoa ya Mwanza, Mbeya, Tanga, Arusha, Ruvuma, Mtwara, Morogoro, Zanzibar na kumalizia na Dar es Salaam.

Akitoa maoni yake baada ya mafunzo hayo, Bi.Doroth ambaye ni mstaafu mtarajiwa yeye amefurahishwa na elimu kuhusu kuwekeza katika hati fungani na kwa elimu aliyoipata hatababaika wapi awekeze fedha zake.

Amewaasa wenzake wanaotarajiwa kustaafu kujihadhari na matapeli kwani wana namna nyingi za hadaa na pindi wanapopata taarifa kutoka kwa mtu ambaye haeleweki watoe taarifa kwenye vyombo vya dola.

“Tujiepushe na watu tusiowafahamu na hata wale tunaowafahamu kwani itasaidia kupoteza fedha utakazolipwa.” Alisema.

MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), CPA. Hosea Kashimba, akitoa hotuba ya kufunga semina hiyo Agosti 5, 2021.
Mkurugenzi wa Uendeshaji, PSSSF, Bw. Mbaruku Magawa akieleza mafao yanayotolewa na Mfuko.
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo.
Bw. Herman Gudluck, Meneja wa Mipango na Uwekezaji, PSSSF, akitoa mada kuhusu uwekezaji wa Mfuko.
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo.







Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"