NA
MWANDISHI WETU
WAZIRI
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye
Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, amewaonya wale wote waliojiandaa kuwatapeli
Watumishi wa Umma wanaotarajiwa kustaafu utumishi wa Umma kuacha mipango hiyo
kwani vyombo vya dola vitawashughulikia kwa mujibu wa sharia za nchi.
Waziri
Mhagama aliyasema hayo leo Agosti 4, 2021, wakati akifungua semina ya mafunzo
kwa wastaafu watarajiwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022, iliyoandaliwa na Mfuko wa
Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwenye ukumbi wa mikutano wa jengo
la Golden Jubilee Towers jijini Dar es Salaam.
“
Baada ya kuanza utaratibu huu wa mafunzo, Serikali ya Awamu ya sita chini ya
Rais wetu, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha nia ya kulinda wastaafu, jambo
hili la kuwatapeli wastaafu tunataka kulikomesha mara moja na tunaomba vyombo
vinavyohusika na vile ambavyo vipo hapa leo ninapofunga mafunzo haya na wao
waanze mkakati wa kubaini matapeli wote ndani ya serikali na nje ya serikali
wanaojihusisha kuangamiza maisha ya wastaafu wetu.” Alisisitiza.
Aliwaasa
wastaafu hao watarajiwa kuwa makini kwa kufuata vyanzo sahihi vya utoaji
taarifa za Mfuko ili kujiepusha na taarifa za watu wenye nia mbaya.
“Ilikuwa
ni kiu yangu mstaafu ajue taarifa zake zote kama ziko sahihi, Mfumo tunaokwenda
kuuzindua leo unakuwezesha mwanachama na msfaatu mtarajiwa kufungua simu yako
na kuangalia michango yako yote iko sahihi? Kuna michango haijapelekwa? Kuna
michango imepelekwa pungufu?...”Alisema
Alisema
Mfumo huo utawawezesha wastaafu watarajiwa kuweka mambo sawa kabla haijafikia
siku ya mwisho ya utumishi wa Umma.
“Ninawaomba
sana mtumie Mfumo huu walau kila baada ya miezi mitatu angalia taarifa zako ili
kuhakikisha ni sahihi.” Alibainisha.
Akizungumzia
kuhusu mafunzo hayo, Mhe. Mhagama alisema mafunzo hayo yanalenga kuwaelimisha
namna bora na sahihi ya kutumia fedha wanazolipwa baada ya kustaafu.
“PSSSF
ilipokea maagizo kutoka serikalini na hasa ile dhamira ya dhati ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kuona ni namna
gani wastaafu wanashirikishwa kupata uelewa wa maisha baada ya kustaafu
nawapongeza Mfuko kwa kutimiza agizo hilo.” Alisema.
…..Ndio
maana mafunzo haya tumeona yaendeshwe nchi nzima ili wastaafu wetu watarajiwa
waliobakiza miaka mitano, mitatu, miwili, mmoja na hata kama wamebakiza miezi
mitatu, wajue ni namna gani wanaweza kufanya matumizi sahihi ya fedha watakazozipata
kama malipo yao ya pensheni baada ya kustaafu.” Alibainisha.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA Hosea Kashimba alisema jumla ya
wastaafu watarajiwa wanaofikia 600 wameshiriki katika mafunzo hayo na kwamba
wanahitimisha awamu ya kwanza ya mafunzo hayo mahsusi kwa wanachama
wanaokaribia kustaafu.
Alisema
semina hizo zimeshafanyika kwenye mikoa mbalimbali zikianza Julai 14, 2021
jijini Dodoma, na kuendelea kwenye mikoa ya Mwanza, Mbeya, Tanga, Arusha,
Ruvuma, Mtwara, Morogoro na Zanzibar ambapo hadi sasa washiriki 3,000
wamehudhuria mafunzo hayo.
Alisema
Mfuko umetimiza miaka mitatu tangu uanzishwe baada ya kuunganishwa kwa mifuko
ya PSPF, PPF, LAPF NA GEPF na kuzaliwa , Mfuko mpya ulirithi madai mengi ya
mafao kutoka katika mifuko iliyounganishwa, madai yote yalilipwa na Mfuko
unaendelea kulipa mafao mbalimbali ya wanachama yale ya kawaida.
Kuhusu
mafunzo hayo CPA Kashimba alisema Mfuko pamoja na majukumu mengine ya msingi
una jukumu kubwa la kuhakikisha unawashauri vema wanachama katika matumizi
sahihi ya fedha za mafao wanazopata baada ya kustaafu.
“Hatuishii
kuwalipa tu mafao na kuwaacha waende tu bila dira ya namna gani wanatumia mafao
yao kwa ufanisi,” alisema na kuongeza……. hivyo semina hizi zinajumuisha kutoa
elimu kwa wastaafu watarajiwa kwenye maeneo ya msingi kama vile wanachama na
michasngo, mafao na mambo mengine ya kuzingatiwa tukiwa katika ajira wakati wa
kustaafu na baada ya kustaafu.”Alifafanua.
Alisema
katika kufanikisha mafunzo hayo Mfuko umeshirikiana na taasisi mbalimbali za
fedha ambazo zinatoa elimu juu ya uwekezaji na matumizi sahihi ya fedha.
Akieleza
zaidi kuhusu uhai wa Mfuko tangu uanzishwa miaka mitatu iliyopita, CPA Kashimba
alisema hadi kufikia Juni 2021, Mfuko ulikuwa na wanachama 705,484 ambao ni
watumishi wa umma na wafanyakazi wa makampuni ambayo serikali inamiliki hisa
zaidi ya asilimia 30% na kwa kipindi hicho mfuko ulikuwa unahudumia wastaafu na
wategemezi 188,330.
“Katika
kipindi cha uhai wa Mfuko miaka mitatu tangu uanzishwe, Mfuko umelipa wanufaika
143,367, jumla ya shilingi Trilioni 5 na kiasi hiki cha fedha kikitumika vizuri
na wanufaika kinaweza kikatoa mchango
mkubwa katika kuendeleza miradi mbalimbali, kutengeneza ajira kwa vijana,
kuongeza pato la mstaafu na hatimaye pato la taifa.” Alibainisha CPA Kashimba.
Kwa
mwezi Julai 2021, umelipa pensheni ya mwezi kw awanufaika 145,417 ya thamani ya
shilingi bilioni 56.
“Tumeona
haja ya kuandaa mpango wa mafunzo maalum kwa ajili ya wanachama wanaotarajia
kustaafu Mafunzo haya yatalenga katika maeneo ya uwekezaji katika viwanda
vidogovidogo, uwekezaji katuika masoko ya fedha.” Alisema
Akizungumza
kwa niaba ya wastaafu watarajiwa, Mwalimu Hussein Masoud aliushukuru Mfuko kwa
kuandaa mafunzo hayo kwani fedha wanazotarajiwa kupokea zinahitaji maelekezo ya
jinsi gani wanaweza kuhifadhi na kutumia fedha hizo vizuri.
0 comments:
Post a Comment