RC KUNENGE APOKEA MISAADA YA VIFAA KWA AJILI YA WANAFUNZI WALIOATHIRIKA KUTOKANA NA BWENI LA WASICHANA SEKONDARI YA KIWANGWA KUTEKETEA KWA MOTO

NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amepokea misaada ya vifaa mbalimbali kuwasaidia wanafunzi waliathirika kutokana na ajali ya moto iliyotokea katika bweni la wasichana shule ya sekondari Kiwangwa iliyoko jimbo la Chalinze Mkoani Pwani majira ya saa 1 usiku Julai 22/2021.

“Tumekuja hapa na wadau ambao wametupatia misada mbalimbali, Jukumu letu la kwanza lilikuwa ni kuhakikisha watoto wetu wako salama, na kwakweli wako salama na tunamshukuru mwenyezimungu hatukuweza kupata madhara ya kuweza kupoteza maisha ukiacha mshtuko walioupata baadhi yao, na jukumu letu la pili ni kuhakikisha kuhakikisha baada ya kuwa salama wanaendelea kupata sehemu ya makazi ili waendelee na masomo.” Alisema RC Kunenge.

Alisema vifaa vya msingi kama magodoro, mashuka, mito, madaftari, na mahitaji mengine ya watoto hao wa kike vimepatikana.

Alisema katika ajali hiyo mabweni mawili ya wasichana yaliteketea kwa moto, na amewashukuru sana wadau hao kutokana na misaada hiyo ambayo katika wakati huu watoto hao wanaweza kuendelea na masomo.

“Bado tunaendelea kupokea misada, tumeelekeza Halmashauri iwe imejenga walau bweni moja ndani ya mwezi mmoja na kuna wabia wengine wametuahidi kujenga bweni la pili, na kwakweli hii ndiyo Tanzania tunayoifahamu tunapokuwa na changamoto tunakuwa kitu kimoja na tunasaidiana.” Alifafanua.

Alisema kutokana na ajali hiyo ambayo sasa ni mara ya pili kutokea, Mkoa umeunda timu kuchunguza chanzo cha moto huo ni nini.

“Tuna historia katika shule hii……, hii ni mara ya pili bweni la watoto wa kike linaungua hivyo tunataka tujue, chanzo ni upande wa ujenzi kwa maana ya utaalamu, au kuna matumizi kwa wale wanaotumia mabweni hayo au labda ni hujuma,” alifafanua.

Alisema mabweni ya sasa yatajengwa kwa kuzingatia utaratibu wa sasa na kuzingatia taratibu za kiusalama kulingana na maelekezo ya TAMISEMI.

“Kubwa ni kwamba watoto wateendelea na masomo, wako kwenye mikono salama kwani urithi mkubwa kwa watoto wetu ni kuwapatia elimu. Na niendelee kumshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa upendo wake kwani metupa pole kutokana na ajali hii.” Alisema.

Pia amempongeza Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete kwa moyo wake wa upendo, kwa kutembelea eneo hilo la ajali nay eye ndiye aliyeanzisha shule hiyo wakati huo akiwa mbunge.

Kwa upande wake, Mbunge wa jimbo la Chalinze, Mhe., Ridhiwani Kiwkete alisema yeye kama mbunge anawahakikishia wanafunzin hao wanarudi kwenye hali yao ya kawaida.

“Nikuhakikishie Mkuu wa Mkoa, mahitaji kuhusiana na wanafunzi yatakayowawezesha kuendelea kusoma yanapatikana.” Alisema

Alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge kwa kuonyesha uongozi kufuatia ajali hiyo.

“Leo ni siku ya kupata uongozi na faraja kutoka kwako na wafadhili wetu waliokuja, tunaamini katika uongozi wako na wewe umetuonyesha uongozi katika kipindi cha matatizo, walionifundisha siasa na uongozi waliniambia kiongozi mzuri anaonekana katika kipindi cha shida na siyo kipindi cha raha na wewe umekuwa mfano bora wa kuigwa na sisi tunaendelea kujifunza kutoka kwako,…haujatuacha siku ya kwanza tulipotokewa na janga hili na umeendelea kuwa nasi leo tunapopokea mahitaji haya.” Alisifu na kuongeza…………………Hakika naiona nguvu yako Mhe. Mkuu wa Mkoa.

Aidha kwa upande Ali Yusuf Abdulrahman Surya, mwenyekiti taasisi ya Miraj-Tanzania, alisema binadamu ana mahitaji mawili ya kiroho na kimwili.

Mahitaji ya kirohoro tunawapatia maneno ya mwenyezimungu ili roho ipate dawa, itulie ifanye ibada na kufanya mwili mwema, na pia kuna mahitaji ya mwili, makazi, mavazi, vyakula na vinginevyo.

“Ombi la Mkuu wa Mkoa la kupata mabweni mawili Inshaallah tunawaahidin kuwa tutajenga.” Aliwahakikishia.




Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"