WAJUMBE WA KIKAO CHA MASHIRIKIANO KATI YA SMZ NA SMT WAKAGUA MIRADI YA SEKTA YA UJENZI
Meneja wa Wakala wa Barabara
Tanzania (TANROADS), mkoa wa Tanga, Mhandisi Alfred Ndumbaro, akitoa Taarifa ya mradi wa
mizani ya Pongwe na Barabara ya Tanga –
Pangani (Km 50), kwa wajumbe wa kikao
cha mashirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT), walipokuwa wakikagua miradi hiyo, mkoani
Tanga.
Muonekano wa Gari la mizigo
likipima uzito katika kituo cha mizani cha Pongwe, mkoani Tanga.
Kiongozi wa zamu katika
Kituo cha mizani cha Pongwe, mkoani Tanga, Elias Magugudi, akielezea namna
huduma za upimaji uzito wa magari zinavyofanyika katika kituo hicho wakati
wajumbe wa kikao cha mashirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walipofika hapo kujionea utendaji
wa mizani hiyo.
Abiria wakiingia katika kivuko cha MV Pangani II kwa ajili ya kuvuka kuelekea upande wa Bweni, Tanga. Kivuko hicho chenye uwezo wa kubeba abiria 100 na magari Sita sawa na tani 50, kinatoa huduma ya usafirishaji kati ya Pangani na Bweni, mkoani Tanga.
Comments
Post a Comment