TUNDU LISSU AFURAHISHWA NA UONGOZI WA RAIS SAMIA NDANI YA SIKU 100

 

Rais Samia Suluhu Hassan

WAKATI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akitimiza siku 100 kama Rais wan chi, Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Mhe. Tundu Lissu amefurahishwa na mambo kadhaa ambayo Rais ameyafanya.

Akihojiwa kwenye kipindi cha Amka na BBC leo asubuhi Juni 29, 2021, Mhe. Lissu alisema mabadiliko makubwa ya kauli na vile vile ile healing ya watu kuna faraja kubwa, taifa limepumua kwa sababu Mamam Samia Suluhu Hassan yuko tofauti sana kwa kauli, anazungumza taratibu hatishii watu, vyombo vya habari vimeanza kuandika vitu ambavyo hawakuwa wakiviandika hapo kabla, alisema.

“Kuna baadhi ya vitu ambavyo amevifanya ambavyo vimeongeza faraja mfano msimamo wake kuhusu ungonjwa wa Covid19 ambao umeua watu wengi duniani nchi ilikuwaimefika mahali  imekwama, mama amebadilisha hiyo hali tunaelekea kwenye ushirikiano na majirani zetu, ushirikiano na Jumuaiya ya Kimataifa na Shirika la Afya Duniani katika kukabiliana na huu ugonjwa unaoikabili dunia nzima hilo ni jambo jema sana.”

“Vilevile mama alisema yeye hataki kuona watu wakikamatwa bila sababu na kufunguliwa kesi za kubambikia na pia ameachilia watu waliokuwa wameshikiliwa kwa muda mrefu wakiwemo masheikh wa Uamsho Zanzibar.” Alisema.

Hata hivyo Mhe. Lissu amehimiza uwepo wa Katiba mpya “Tulitakiwa tuwe na Katiba mpya baada ya tume ya Rais iliyoleta nchi kwenye mfumo wa vyama vingi , tume ya Jaji Nyalali iliyopendekeza tuwe na Katiba mpya mwaka 1991 hili suala la Katiba mpya lilipaswa liwe siyo swala la kujadiliwa leo.” Alisema.

Akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam Jumatatu Juni 28, 2021 Rais Samia aliwaahidi watanzania kuwa Katiba mpya ni suala muhimu lakini kwa sasa ameomba apewe muda kulishughulikia.

Mhe. Tundu Lissu
“Naomba nipeni muda nisimamishe nchi kwanza kiuchumi tuite wawekezaji wawekeze, ajira zipatikane uchumi ufunguke halafu tutashughulikia mengine, tutashughulikia katiba, hiyo mikutano ya hadhara wakati ukifika, lakini sasa hivi tumeruhusu vyama vya siasa kufanya mikutano na watu wao mikutano ya ndani na ninadhani mmeona.” Alibainisha Mheshimiwa Rais Samia.

Rais Samia aliapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Machi 19, 2021 kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tano marehemu Dkt. John Pomba Magufuli Machi 17, 2021.

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"