RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI WAKATI AKITIMIZA SIKU 100 TANGU AINGIE MADARAKANI

 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo Juni 28, 2021 amekutana na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakati akitimiza siku 100 tangu aingie madarakani, Mhe. Rais alianza mkutano wake kwa kupokea maoni na maswali kutoka kwa Wahariri wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bw. Deodatus Balile.

Baada ya kupokea maoni na maswali hayo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa alitoa hotuba fupi na kumkaribisha Mhe. Rais ambaye alijibu maswali hayo na kuelezea dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita anayoiongoza kuwa itashirikiana kwa karibu na vyombo vya habari katika kutekeleza majukumu yake na kwa kuonyesha hilo, Rais ameagiza magazeti ambayo yalimaliza adhabu yake ya kufungiwa yatakapokamilisha usajili yaachiwe yaendelee na jukumu lake la kuhabarisha.

Rais pia ametoa changamoto kwa vyombo vya habari kuchangamkia fursa za matangazo kutoka Taasisi za Umma na Binafsi na kuwaondoa shaka kuwa hakuna mahala popote ambapo serikali ilitoa maelekezo maalum ya kuvinyima vyombo vya habari vya binafsi matangazo ya biashara kutoka serikalini.




 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bw. Deodatus Balile akizungumza

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"