MAKONSELI WAKUU WA MSUMBIJI NA OMAN WAWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO
Na mwandishi wetu.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata
Mulamula apokea nakala ya hati za utambulisho za Makonseli Wakuu wawili kutoka
Msumbiji na Oman wenye makazi Zanzibar.
Makonseli
hao ni Mhe. Agustinho Abacar Trinta Konseli Mkuu wa Msumbiji pamoja na Mhe.
Said Salim Al Sinawi Konseli Mkuu wa Oman
Pamoja
na mambo mengine, viongozi hao wamedajiliana masuala mbalimbali ya kuimarisha
uhusiano wa Kidiplomasia na Kiuchumi baina ya nchi zao na Tanzania.
Konseli Mkuu wa Oman mwenye makazi Zanzibar Mhe. Said Salim Al Sinawi akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasilisha nakala ya hati za utambulisho
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokea nakala ya hati za utambulisho
kutoka kwa Konseli Mkuu wa Oman mwenye makazi Zanzibar Mhe. Said Salim Al
Sinawi. Uwasilishwaji wa hati hizo umefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara
jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Konseli Mkuu wa
Msumbiji mwenye makazi Zanzibar Mhe. Agostinho Abacar Trinta katika Ofisi ndogo
za Wizara jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasilisha nakala ya hati za
utambulisho
Comments
Post a Comment