RC KUNENGE ATOA ONYO KWA WATENDAJI WA BODI YA MAGHALA NA WAKALA WA VIPIMO

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge ametoa Onyo  kwa watendaji wa Bodi ya Maghala na Wakala wa Vipimo kwa kushindwa kupima mizani zilizopo kwenye  maghala ya Msingi  zinazotumika kupokelea Ufuta na  kushindwa kusimamia maandalizi ya Maghala Makuu, hali inayopelekea kero na kusuasua kwa zao hilo.

Ameyasema hayo leo Mei, 26 2021 wakati akiendesha Mkutano wa Wadau wa Ufuta Mkoani hapo, Mkutano huo umefanyika Ikwiriri Wilayani Rufiji.

"Natoa Onyo kwa  watendaji wa Serikali siihitaji Ubabaishaji' Changamoto katika zao la  ufuta chanzo pia ni ninyi  Watumishi wa Serikali.

Amesema hafurahishwi  na Watendaji hao wa Serikali kusubiri kuitwa na  Wakulima badala ya kuwafuata na kutoa huduma. Ameeleza hatosita kuwaondoa Mkoani hapo kwa kushindwa kusimamia wajibu wao kikamilifu.

Aidha, RC Kunenge ametoa siku tatu kwa watendaji hao  kwamba hadi kufikia Mei 28, 2021 kuhakisha kuwa wanakamilisha maandalizi ya Maghala  Makuu na Upimaji wa Mizani kwenye maghala ya Msingi.


 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"