RAIS SAMIA "AMTUMBUA" MKURUGENZI MKUU TPA DEUSDEDIT KAKOKO
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amemsimamisha kazi MKURUGENZI MKUU wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Bw. Deusdedit Kakoko ili kupisha uchunguzi.
Rais Samia ametangaza uamuzi huo leo Machi 28, 2021 wakati akipokea ripoti ya mdhibiti na mkaguzi MKUU wa hesabu za serikali (CAG) ya mwaka 2019/2020 na ile ya Taasisi ya Kuzuia na kudhibiti Rushwa (TAKUKURU) Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo Machi 28, 2021.
Comments
Post a Comment