TANZANIA INAZIADA YA UMEME MEGAWATI 424.28

NA K-VIS BLOG, MOROGORO

TANZANIA kwa sasa inazalisha umeme Megawati 1, 604.81 kwa siku na mahitaji ya juu kabisa ya umeme nchi nzima ni Megawati 1,180.53, na hivyo kufanya kuwepo kwa ziada ya umeme Megawati 424.28, Meneja Mwandamizi wa Uzalishaji Umeme (power generation) kutoka Shirika la Umeme Nchini TANESCO, Mhandisi Stephen Manda (pichani juu) amesema.

Akiwasilisha mada kuhusu moja ya jukumu la TANESCO la kuzalisha umeme (Generation) kwenye kikao kazi cha TANESCO na Wahariri Waandamizi wa vyombo vya habari leo Februari 26, 2021 kwenye ukumbi wa NSSSF mkoani Morogoro alisema TANESCO inazalisha Megawati 1,393.45 na wazalishaji binafsi wanachangia kiasi cha Megawati 211.36.

Akifafanua zaidi, Mhandisi Manda alisema Gridi ya Taifa inabeba umeme Megawati 1,567.951 ambapo asilimia 87 ya umeme huo unazalishwa na TANESCO huku asilimia 33.126 unatoka kwa wazalishaji binafsi.

Mhandisi Manda alisema, ni matatrajio ya taifa kuwa mradi mkubwa wa umeme wa Julius Nyerere wa Megawati 2115 utaleta ongezeko kubwa la umeme na hivyo kuleta nafuu kubwa ya gharama za umeme na hivyo pato la taifa na wananchi kwa ujumla. Aidha alisema kwa sasa umeme wa Gesi ndio unaongoza kwa kuchangia kiasi kikubwa cha umeme kwa asilimia 56, huku umeme wa maji ukichangia asilimia 36, mafuta asilimia 7 umeme utokanao na taka asilimia 1.

Meneja Mwandamizi wa Uzalishaji Umeme (power generation) kutoka Shirika la Umeme Nchini TANESCO, Mhandisi Stephen Manda
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka akifuatilia majadiliano
Steven Chuwa, Mhariri wa ITV
Scholastica Mazula, Mhariri wa EFM-ETV
Bw. Ramadhan Mpenda, Mhariri wa Habari TBC1
Bw. Masoud Kipanya kutoka Clouds Media Group
Bw.Fred Mwanjala, (kushoto) Afisa Habari Mwandamizi MAELEZO na Bi. Lilian Timbuka, Mhariri Mwananchi
Bw.Eckland Mwafisi, Mhariri LAJIJI
Bw. Mgaya Kingoba, Mhariri wa Habari gazeti la Habari Leo
Meneja Uhusiano TANESCO Bi. Johary Kachwamba  akipitia  nyaraka wakati mkutano ukiendelea
Bw. Philemon Lusekelo, Mhariri wa Habari Gazeti la The Guardian
Bw. Bernard James, Mhariri wa Star TV/na Radio Free Africa
Bw. Said Mwinshehe (kulia) Mhariri Mkuu wa Michuzi TV/Michuzi Blog akiwa na Edwin Kamugisha Kamugisha

Joseph Mwendapole wa Nipashe
Kutoka kushoto ni Bi. Eshe Muhidin kutoka TBC1, Fred Mwanjala kutoka MAELEZO na Bi. Lilian Timbuka kutoka Mwnaanchi Communications.
Mkurugenzi Mtendaji TANESCO. Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja

 Bi. Johary Kachwamba, Meneja Uhusiano TANESCO akizungumza kwenye mkutano huo.




Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"