TANESCO YAJA NA MFUMO "MTEJA UKINUNUA UMEME HULAZIMIKI KUINGIZA TOKEN KWENYE MITA, UNAINGIA WENYEWE MOJA KWA MOJA BAADA YA MALIPO"

 

SHIRIKA la Umeme nchini TANESCO linatarajia kuweka mfumo utakaomuwezesha mteja aliyenunua umeme kupitia simu ya kiganjani kutolazimika kuingiza namba (TOKEN) kwenye mita na badala yake umeme utaingia moja kwa moja kwenye mita  mara tu baada ya kukamilisha malipo.

Meneja Mwandamizi Usambazaji Umeme Mhandisi Athanasius  Nangali(pichani juu) amewaambia Wahariri wa vyombo vya habari wanaoshiriki kikao kazi baina ya TANESCO na Wahariri mjini Morogoro Februari 26, 2021.

“TANESCO tunaendelea kuboresha zaidi utoaji wa huduma zetu na sasa hivi tuko kwenye mpango wa kuweka mfumo ambapo mteja atakaponunua umeme kwenye simu yake au kwingineko basi umeme utaingia moja kwa moja kwenye mita yake nyumbani na hatalazimika tena kuingiza namba (TOKEN) kwenye mita.” Mhandisi Nangali amefafanua.

Akifafanua zaidi alisema TANESCO tayari imemuajiri mtaalamu mshauri kutoka serikalini ili akague specification na akishamaliza kuzikagua tunaingia kwenye huo mfumo moja kwa moja.

“Lengo letu sisi tunataka wateja wetu wapate huduma ya umeme bila matatizo yoyote”. Alifafanua.


Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"