YOUNG WOMEN LEADERSHIP YATOA MAFUNZO YA LISHE KWA WATOA HUDUMA YA AFYA NGAZI YA JAMII

 

Afisa Miradi wa Shirika la Young Women Leadership (YWL), Veronica Massawe akizungumza wakati wa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma ya afya ngazi ya jamii kutoka Kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Shirika la Young Women Leadership ‘YWL’ linalojihusisha na utetezi wa haki za wanawake, vijana na watoto limetoa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma ya afya ngazi ya jamii ili waweze kuelimisha wazazi au walezi wenye watoto kuanzia mwaka 0 hadi 6 kwa lengo la kuimarisha kinga ya mwili na afya kwa watoto chini ya umri wa miaka 6.
Akizungumza leo Alhamis Oktoba 1,2020 wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Shinyanga Fairies Hotel, Afisa Lishe wa Manispaa ya Shinyanga, Joanitha Jovin aliwataka watoa huduma ya afya ngazi ya jamii kufikisha elimu hiyo kwa walengwa ili kuwasisitiza wazingatie lishe bora kwa watoto wao.
“Kupitia mafunzo haya nendeni mkawaelimishe wazazi na walezi wenye watoto kuanzia mwaka 0 hadi 6 mliowabaini kupitia  kaya hadi kaya kwenye maeneo yenu kuhusu njia rahisi na rafiki za ku Kadama Malunde 1 message No attachment Oct 1 TGNP YAWAPIGA MSASA WASAIDIZI WA KISHERIA KUKABILIANA NA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO
Msajili Msaidizi wa Watoa Huduma za Kisheria mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale akizungumza wakati akifungua mafunzo kwa Wasaidizi wa Kisheria kutoka wilayani Kahama yaliyolenga kuwajengea uwezo wa namna ya kukabiliana na masuala ya ukatili wa kijinsia hasa yanayowakumba wanawake na watoto leo Alhamis Oktoba 1,2020. Mafunzo hayo yameandaliwa na Shirika la TGNP na UNFPA kwa kushirikiana na PACESHI. Kulia ni Meneja Mradi wa Huduma ya Msaada wa Kisheria  kupitia Wasaidizi wa Kisheria (Paralegals) John Shija kutoka Shirika la PACESHI Shinyanga mjini, kulia ni Mwezeshaji katika mafunzo hayo,Mwanasheria Neema Ahmed. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Afisa Miradi wa Shirika la Young Women Leadership (YWL), Veronica Massawe akizungumza wakati wa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma ya afya ngazi ya jamii kutoka Kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Shirika la Young Women Leadership ‘YWL’ linalojihusisha na utetezi wa haki za wanawake, vijana na watoto limetoa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma ya afya ngazi ya jamii ili waweze kuelimisha wazazi au walezi wenye watoto kuanzia mwaka 0 hadi 6 kwa lengo la kuimarisha kinga ya mwili na afya kwa watoto chini ya umri wa miaka 6.
Akizungumza leo Alhamis Oktoba 1,2020 wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Shinyanga Fairies Hotel, Afisa Lishe wa Manispaa ya Shinyanga, Joanitha Jovin aliwataka watoa huduma ya afya ngazi ya jamii kufikisha elimu hiyo kwa walengwa ili kuwasisitiza wazingatie lishe bora kwa watoto wao.
“Kupitia mafunzo haya nendeni mkawaelimishe wazazi na walezi wenye watoto kuanzia mwaka 0 hadi 6 mliowabaini kupitia  kaya hadi kaya kwenye maeneo yenu kuhusu njia rahisi na rafiki za kuimarisha lishe bora kwa akina mama wajawazito,wanaonyonyesha na wenye watoto chini ya umri wa miaka 6”,alisema Joanitha.
Naye Afisa Miradi wa Shirika la Young Women Leadership (YWL), Veronica Massawe amesema mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa "Uwajibikaji Jamii kwa watoto na familia" (Community Action For Children and Families) unaotekelezwa na YWL katika vijiji vitatu vya Kata ya Mwawaza ambavyo ni Mwawaza, Negezi na Bugimbagu kwa muda wa mwaka mmoja (Agosti 2020 – Julai 2021) kwa ufadhili Shirika la Firelight Foundation la nchini Marekani.
Alisema lengo la mradi huo ni kuziwesha familia 600 katika kaya ya Mwawaza ili kuimarisha kinga ya mwili,afya ya watoto na familia pamoja na  uchumi wa familia kwa kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza kilimo cha vyakula lishe ikiwemo matunda na mbogamboga ambapo walengwa ni wazazi au walezi wenye watoto kuanzia umri wa mwaka 0 hadi miaka 6.
“Miongoni mwa majukumu ya watoa huduma za afya ngazi ya jamii ni kuwafuata walengwa wa mradi kaya hadi kaya na kuwaelisha kuhusu lishe kwa wajawazito na wanawake wanaonyesha,unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee ndani ya miezi 6 ya mwanzo ili kuimarisha kinga ya mwili na afya ya mtoto na vyakula vya nyongeza kwa mtoto kuanzia miezi 6 ya mwanzo”,alifafanua Veronica.
Alisema elimu nyingine ni kuhusu usafi na usalama wa maji na mazingira,malezi na makuzi bora ya mtoto na masuala ya kijinsia katika malezi ya mtoto sambamba na kuwafundisha na kuwaanzishia bustani za mboga mboga,matunda na vyakula lishe ili kuimarisha lishe kwa watoto wenye umri chini ya miaka 6 na kukuza kipato cha familia.
Afisa Lishe wa Manispaa ya Shinyanga, Joanitha Jovin akitoa elimu ya lishe wakati wa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma ya afya ngazi ya Jamii kutoka Kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Oktoba 1,2020.
Afisa Lishe wa Manispaa ya Shinyanga, Joanitha Jovin akitoa elimu ya lishe wakati wa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma za afya ngazi ya Jamii kutoka Kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Miradi wa Shirika la Young Women Leadership (YWL), Veronica Massawe akizungumza wakati wa mafunzo ya lishe kwa watoa huduma za afya ngazi ya Jamii kutoka Kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"