ERB YARIDHISHWA NA UJENZI WA MIRADI YA KIMKAKATI

NA MWANDISHI WETU, MOROGORO

BODI ya Usajili wa Wahandisi nchini (ERB), imeridhishwa na kazi za ujenzi wa miundombinu ya kisasa na kimkakati inayojengwa mkoani Morogoro kwa kuwa imezingatia viwango vya kihandisi, na ubora unaowiana  na thamani ya fedha.

Msajili wa Wahandisi Eng. Patrick Barozi amesema hayo alipokagua miradi ya kimkakati ya soko la kisasa la Manispaa ya Morogoro, machinjio ya kisasa ya Nguru Hills Ranch na miundombinu ya umwagiliaji katika  shamba la miwa la Mbigiri katika kiwanda cha miwa cha Mkulazi.

“Tunawapongeza wahandisi waliofanyakazi katika miradi hii kwa kuwa wabunifu na kuzingatia weledi na viapo vyao hali itakayosababisha miradi hii kukamilika kwa wakati na kutioa fusra za ajira, elimu na biashara kwa wananchi”, amesema Eng. Barozi.

Amesema ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na wahandisi ni sehemu muhimu ya majukumu ya ERB lakini pia zoezi hilo ni fusra kwa wahandisi waliopo katika mafunzo kujifunza na kubadilishana uzoefu na changamoto na wahandisi walioko kwenye miradi na hivyo kuwajengea uwezo wahandisi wapya.

Eng. Barozi ametoa wito kwa vyuo vikuu nchini kuongeza udahili wa wanafunzi katika fani zenye upungufu wa wataalam ili kuepuka kutumia fedha nyingi kuajiri wataalam kutoka nje ya nchi.

Nae msimamizi wa ujenzi wa soko la Manispaa ya Morogoro  Eng. Juma Gwisu amesema ujenzi wa soko hilo umekamilika kwa asilimia 99 na kazi inayoendelea ni kuwapanga wafanyabiashara katika maeneo yao.

Zaidi ya wafanyabiashara elfu mbili wanatarajiwa kunufaika kwa kufanyabiashara katika soko hilo la kisasa lililogharimu zaidi ya shilingi bilioni 17.

 

Kwa upande wake Meneja wa ujenzi wa ranch ya Nguru Hills Eng. Grayson Bambanza amesema machinjio  ya ranch hiyo iko katika hatua za mwisho za ukarabati mkubwa utakaowezesha kuzalisha nyama itakayouzwa katika masoko ya kimataifa na hivyo kutoa fursa nyingi za ajira kwa wataalam wa mifugo na kilimo nchini,  kuongeza biashara ya kununua mifugo na mazao ya shambani toka kwa  wakulima na wafugaji na hivyo kukuza uchumi wa jamii mkoani Morogoro.

“Takriban ng’ombe mia moja na mbuzi na kondoo mia mbili watakuwa wakichinjwa kila siku katika ranch hiyo itakapokamilika na asilimia 80 ya nyama kuuzwa nje ya nchi na asilimia 20 pekee ndio itauzwa nchini” amsesisitiza Eng. Bambanza.

Meneja  umwagiliaji wa  shamba la miwa la Mbigiri katika Kiwanda cha sukari Mkulazi Eng. Juvenal Matumaini amesema kukamilika kwa mabwawa ya umwagiliaji katika kiwanda hicho kutawezesha kuanza kwa uzalishaji wa sukari wa kiwanda hicho kinachotarajiwa kutoa ajira zaidi ya elfu tatu na mia sita kitakapoanza.

Kiwanda cha sukari Mkulazi kinachomilikiwa kwa ubia kati ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), na Jeshi la Magereza kiko katika hatua za mwisho kuanza uzalishaji na kinatarajiwa kuzalisha tani elfu hamsini za sukari kwa mwaka kitakapoanza kazi na hivyo kuongeza uzalishaji wa sukari nchini na kutoa fursa nyingi za ajira.

Msajili wa wahandisi Eng. Patrick Barozi akisisitiza jambo kwa wahandisi wanaosimamia  ukarabati mkubwa wa machinjio ya kisasa katika ranch ya Nguru Hills Mvomero mkoani Morogoro



Ujenzi wa mifereji ya kupitisha maji kwenda kwenye mabwawa ya kumwagilia miwa katika shamba la miwa la Mbigiri ukiendelea, shamba hilo ni sehemu ya mashamba yanayomilikiwa na kiwanda cha sukari cha Mkulazi mkoani Morogoro.

Msimamizi wa ujenzi wa soko la Manispaa ya Morogoro Eng. Juma Gwisu akifafanua jambo kwa wahandisi kutoka Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), walipokagua maenedeleo ya ujenzi wa soko hilo.

Muonekano wa nje wa soko la kisasa la Manispaa ya Morogoro ambalo ujenzi wake umekamilika.

Muonekano wa machinjio ya kisasa katika ranch ya Nguru Hills Mvomero mkoani Morogoro

 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"