BILIONI 12 ZA WAKULIMA WA KAHAWA KULIPWA KESHO

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (kushoto) akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Prof.Riziki Shemdoe (kulia) wakati wa kikao kilichojadili ulipwaji wa madeni ya wakulima wa zao la kahawa kwa vyama vikuu vya ushirika KDCU na KCU utakaonza kesho .Kikao kimefanyika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza .

 Picha ya pamoja kati ya Makatibu Wakuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya ( wa pili kushoto)  akiwa kwenye kikao leo Mwanza kujadili kuanza kulipwa kwa wakulima wa Kahawa Kagera.Wengine ni Bw.Emanuel Tutupa (RAS Mwanza) katikati,Prof.Riziki Shemdoe ( Katibu Mkuu Viwanda) na Prof.Faustin Kamuzola (RAS Kagera aliyevaa kofia).

 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (katikati) akiongea na waandishi wa habari leo jijini Mwanza kutangaza uamuzi wa kuanza kuwalipa wakulima wa kahawa wa mkoa wa Kagera fedha zao shilingi Bilioni 12 kupitia Vyama Vikuu vya KDCU na KCU.Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Prof.Riziki Shemdoe.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (pichani) leo ametangaza kuanza kulipwa kwa shilingi Bilioni 12 za wakulima wa kahawa mkoa wa Kagera kupitia Vyama vikuu vya Ushirika KDCU na KCU.

 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella ( katikati) akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (kushoto) na Katibu Mkuu Viwanda na Biashara Prof.Riziki Shemdoe (kulia) leo wakati wa kikao cha kujadili ulipwaji wa madeni ya wakulima wa kahawa mkoa wa Kagera kilichofanyika Mwanza na kuhusisha viongozi wakuu wa Vyama vya Ushirika KDCU na KCU.

 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"