KATIBU MKUU KILIMO AKABIDHI GARI BODI YA PARETO
Mkulima wa mbegu bora za mahindi Bw.Aron Nguma (kulia) wa Arusha
akikabidhi mahindi yaliyokauka ya mbegu kwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo
Bw.Gerald Kusaya leo alipotembelea shamba hilo Ngaramtoni kukagua hali ya
uzalishaji mbegu za mahindi,maharage na ngano .Shamba hilo linamilikiwa na
Wakala wa mbegu Nchini (ASA)
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya (kushoto) akikabidhi
funguo za gari Toyota H/Top kwa Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Pareto Lucas Ayo jijini Arusha. Gari hiyo imekabidhiwa ili kusaidia bodi kuhamasisha wakulima
wengi kulima zao la pareto nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pareto Lucas Ayo akionyesha funguo za
gari mara baada ya kukabidhiwa toka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald
Kusaya (kushoto). Hafla hiyo ilifanyika jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (katikati) akitoa
maelekezo kwa dereva wa Bodi ya Pareto Venance Haule (kushoto) leo
alipokabidhi gari kwa bodi hiyo jijini Arusha .
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (wa saba toka kushoto)
akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa wizara na taasisi zake zilizopo
Arusha alipokabidhi gari kwa Bodi ya Pareto nchini.
Comments
Post a Comment