KATIBU MKUU KILIMO AKABIDHI GARI BODI YA PARETO

Mkulima wa mbegu bora za mahindi Bw.Aron Nguma (kulia) wa Arusha akikabidhi mahindi yaliyokauka ya mbegu kwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya leo alipotembelea shamba hilo Ngaramtoni kukagua hali ya uzalishaji mbegu za mahindi,maharage na ngano .Shamba hilo linamilikiwa na Wakala wa mbegu Nchini (ASA)

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya (kushoto) akikabidhi funguo za gari Toyota H/Top kwa Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Pareto Lucas Ayo  jijini Arusha. Gari hiyo imekabidhiwa ili kusaidia bodi kuhamasisha wakulima wengi kulima zao la pareto nchini.

 

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pareto Lucas Ayo akionyesha funguo za gari mara baada ya kukabidhiwa  toka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya (kushoto). Hafla hiyo ilifanyika jijini Arusha.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (katikati) akitoa maelekezo  kwa dereva wa Bodi ya Pareto  Venance Haule (kushoto) leo alipokabidhi gari kwa bodi hiyo jijini Arusha .


 

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (wa saba toka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa wizara na taasisi zake zilizopo Arusha  alipokabidhi gari kwa Bodi ya Pareto nchini.

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"