Posts

WAZIRI MKUU AFUNGA MAFUNZO YA UHAMIAJI, AHIMIZA UADILIFU

Image
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wahitimu 521 wa mafunzo ya Kozi Na. 01/2023 wakatumie vema ujuzi na maarifa waliyoyapata katika kudhibiti vitendo vya uhalifu hususan maeneo ya vipenyo, vituo na mipakani. Ametoa wito huo leo Ijumaa (Septemba 29, 2023) alipofunga mafunzo hayo kwa askari wa Uhamiaji katika Chuo cha Mafunzo ya Uhamiaji cha Raphael Kubaga, Wilayani Mkinga, katika Mkoa wa Tanga.  Waziri Mkuu amemshukuru Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza kwa vitendo mpango wake wa kuvijengea uwezo vyombo vya ulinzi na usalama nchini. Mheshimiwa Majaliwa pia amewataka wahitimu hao wakafanye kazi kwa uzalendo, weledi na kutanguliza kwanza maslahi ya Taifa katika kazi zao za kila siku. “Kila mmoja akazingatie maadili na miiko ya kazi na akawe mfano bora wa uadilifu katika kituo atakachopangiwa,” amesisitiza. Aidha, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa Jeshi la Uhamiaji wawachukulie hatua kali za kisheria wahitimu ambao watabainika kuwa wanajihusisha na vitend

SERIKALI YASAINI MIKATABA MIWILI YA MSAADA YENYE THAMANI YA BILIONI 50.13 KUNUSURU KAYA MASIKINI

Image
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (kulia) na Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Mhe. Didier Chassot (kushoto), wakisaini hati ya makubaliano ya msaada wa Dola za Marekani milioni 18 (sawa na shilingi bilioni 44.4 za Tanzania), kwa ajili ya kufadhili mpango wa kunusuru kaya maskini awamu ya pili (PSSN II) unaosimamiwa na TASAF katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (kushoto) na Balozi wa Jamhuri ya Ireland nchini Tanzania, Mhe. Mary O’neil (kulia), wakisaini hati ya makubaliano ya msaada wa Dola za Marekani milioni 2.3 (sawa na shilingi bilioni 5.6 za Tanzania), kwa ajili ya kufadhili mpango wa kunusuru kaya maskini awamu ya pili (PSSN II) unaosimamiwa na TASAF. katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (kulia) na Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Mhe. Didier Chassot (kushoto), wakibadilishana hati

MAONESHO YA MADINI GEITA: NAIBU GAVANA BOT DKT. YAMUNGU KAYANDAMBILA ATEMBELEA BANDA LA PSSSF

Image
  Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Yamungu Kayandabila (anayezungumza pichani kulia), ametembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF), kwenye Maonesho ya 6 ya Teknolojia ya Madini, kwenye viwanja vya EPZA, Bombambili mjini Geita. Akiwa katika banda hilo, Dkt. Kayandabila, ambaye alifuatana na Meneja Uhusuano BoT, Bi. Vicky Msina, alipokelewa na Meneja wa PSSSF,  Kanda ya Magharibi, Bw.  Geofrey Kolongo. Bw. Kolongo alimueleza huduma zilizotolewa na PSSSF kwa wananchi na wanachama wa PSSSF ambao ni watumishi wa umma, waliotembeela banda hilo ambapo alisema, wanachama waliweza kupatiwa taarifa kuhusu uanachama wao ikiwa ni pamoja na kupata taarifa za Michango, taarifa za Mafao yatolewayo na Mfuko, wastaafu waliweza kujihakiki kwa kutumia alama za vidole lakini pia walielimishwa jinsi ya kutumia huduma ya PSSSF kiganjani, ambayo inamuwezesha mwanachama na mwajiri kupata taarifa na huduma mbalimbali za Mfuko. Pia wanachama na wananchi walipati

STAMICO KUWAPA MAFUNZO WANACHAMA WA TAWOMA

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) akizungumza na wanachama wa cha cha wachimabaji madini wanawake Tanzania TAWOMA katika mkutano wa kijadiliana Changamoto na mafanikio ya ushiriki wa wanawake katika shughuli za uchimbaji madini ukiofanyika. Kwenye viwanja vya EPA Bombambili mjini Geita.  Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya uchimbaji Madini ya Dhahabu ya BUCKREEF Amelda Msuya akifurahia jambo na Afisa Mawasiliano wa Shirika la Madini la Taifa STAMICO wakati wa mkutano wa TAWOMA uliofanyika kwenye ukumbi wa mkapa katika maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya EPZ Bombambili mjini Geita.  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dorothy Gwajima, wa pili kutoka kulia akifuatilia mkutano huo kwa kuandika mambo muhimu yaliyoainishwa na wachimabaji madini wanawake.  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa GGR Sarah Masasi katika mkutano huo.  ..

VIONGOZI NENDENI MKASIKILIZE WANANCHI-DKT. DOTO BITEKO

Image
 Teresia Mhagama na Godfrey Lulinga  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewataka viongozi wa ngazi mbalimbali nchini kwenda kwenye maeneo ya wananchi kwa ajili ya kutoa huduma, kusikiliza kero zao na kuzitatua. Amesema hayo tarehe 28 Septemba, 2023 katika Kijiji cha Nyakanazi Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera akiwa njiani kuelekea wilayani Ngara kuwasha umeme vijijini pamoja na kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Nishati kutoka nchi za Tanzania, Burundi na Rwanda wanaohusika na Mradi wa umeme wa Rusumo utakaozalisha megawati 80.  “Viongozi wenzangu tutoke maofisini na tuwafuate wananchi walipo, haina maana yoyote kama kuna kiongozi hapa na kuna shida ipo na haijawahi kutatuliwa, Mhe, Rais anachotaka ni wananchi hawa kusikilizwa na kama kuna kero sisi tuzimalize kabla yeye hajaja, wananchi wakisema kuna shida sisi tuzimalize, yeye kazi yake kubwa ni kutafuta fedha kwa ajili ya maendeleo.” Amesema Dkt.Biteko Aidha, Dkt. Biteko ameendelea kusisitiza kuhusu matumizi s

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA SEPTEMBA 29, 2023

Image