Posts

TANAPA YAKUBALI KUANZISHA KITUO KIDOGO CHA ASKARI WA UHIFADHI KATA YA KIHANGA - KARAGWE KUDHIBITI UVAMIZI WA TEMBO.

Image
 Karagwe - Kagera. Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa amefikia makubaliano na Shirika la Hifadhi ya Taifa Tanzania - TANAPA kuanzisha kituo Kidogo cha askari wa uhifadhi katika kata ya Kihanga wilaya Karagwe ili kudhibiti uharibifu unaofanywa na tembo na wanyama wengine wakali wanaoshambulia Wananchi na mali zao mara kwa mara. Makubaliano hayo yamefikiwa leo tarehe 30, Januari 2023 wakati Bashungwa akisikiliza na kutatua kero za wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Kibwera kata ya Kihanga wilaya ya Karagwe. Bashungwa ameitaka Halmashauri ya wilaya Karagwe kushirikiana na TANAPA kutoa elimu kwa jamii na kuuunda Vikundi vitakavyokuwa vinashirikana na askari wa Uhifadhi watakaokaa katika kata hiyo kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi na mali zao. Amemtaka Kamishina Msaidizi wa TANAPA Kanda ya ziwa kukamilisha taratibu wa Kulipa fidia kwa wananchi kata Kihanga ambao wameharibiwa mali zao kwa kuvamiwa na tembo ili waweze kupatiwa kifuta machozi kulingana

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus azungumza na Wanahabari, Ikulu Jijini Dar es Salaam

Image
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus akizungumza na kuwaelezea Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyofanya Davos nchini Uswizi tarehe 16-20 Januari,2023 pamoja na Dakar nchini Senegal tarehe 25-27 Januari, 2023 katika Mkutano uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Januari, 2023. Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus akizungumza na kuwaelezea Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyofanya Davos nchini Uswizi tarehe 16-20 Januari,2023 pamoja na Dakar nchini Senegal tarehe 25-27 Januari, 2023 katika Mkutano uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Januari, 2023. Waandishi wa Habari wakiwa kwenye Mkutano uliohusu Mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyofanya Davos nchini Uswizi (tarehe 16-20 Januari,2023) pamoja na Dakar

DKT MABULA ATAKA MAFUNZO YA MAADILI KWA MADALALI

Image
  Na   Munir Shemweta, WANMM Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameataka kutolewa mafunzo ya maadili kwa Mawakala wa Mali Zisizohamishika (MADALALI) Dkt Mabula amesema hayo leo tarehe 30 Januari 2023 wakati akifungua Mafunzo ya muda mfupi ya Mawakala wa Mali Zisizohamishika (MADALALI) yanayoendeshwa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kwa kushirikiana na Chama cha Mawakala wa Mali Zisizohamishika (AREA) yanayofanyika jijini Dar es Salaam. Alisema, pamoja na mafunzo yanayotolewa kuwa ya kitaalamu zaidi lakini upo umuhimu mkubwa wa kutolewa  mafunzo yanayohusu maadili kwa kuwa eneo hilo limekuwa likisababisha malalamiko  mengi kwa jamii. Alitolea mfano wa Mawakala kuchukua kamisheni toka pande zote zinazohusika kwenye mauziano au upangaji nyumba na kubainisha kuwa suala hilo limekuwa kichocheo cha kupanda bei au kodi za nyumba na kuzidi viwango vya soko lengo likiwa kujipatia kamisheni kubwa na hivyo kuvuruga mwenendo wa soko la milki nchini. Kwa mujibu wa

RAIS SAMIA AKUTANA NA MKURUGENZI WA EGPAF

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kimataifa la Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation (EGPAF) linaloshughulikia kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, Chip Lyons Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Januari, 2023.  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU JANUARI 30, 2023

Image
 

MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2022

Image
Kupata matokeo ya mtihani wa kidato Cha NNE 2022 bonyeza link hapo chini👇 https ://matokeo.necta.go.tz/csee2022/index.htm