Posts

SERIKALI YAJIPANGA KUIMARISHA USAFIRI MAJINI

Image
  WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amesema Serikali imejipanga kuhakikisha inafanya mapinduzi makubwa katika kuboresha usafiri wa majini kwa kujenga meli na kusomesha wataalam anuai wa fani  ya bahari. Akizungumza katika mahafali ya kwanza ya kozi ya ubaharia ambayo yamefadhiliwa na Taasisi ya Ushoroba wa Kati (CCTTFA) jijini Dar es  Salaam amewataka wahitimu wa kozi hiyo, kuwa na nidhamu ili ujuzi  walioupata uwe na manufaa kwa taifa na nchi za ushoroba wa kati kwa ujumla. “Baharia mzuri ni yule mwenye nidhamu anapokuwa akitekeleza majukumu yake, maono na anayezingatia usalama wake, chombo na mali kwa ujumla,” amesisitiza. Aidha amekitaka Chuo cha Bahari (DMI) kuhakikisha kinakuza mtandao wake na taasisi mbalimbali duniani ili kuwawezesha wanafunzi wa chuo hicho kupata muda wa kutosha wa kufanya mazoezi ya vitendo melini (Sea time). Hata hivyo, Prof. Makame ameupongeza wakala wa ushoroba wa kati kwa kuwafadhili wanafunzi hao na kuahidi kutilia mkazo wa kuwa na mpango

UGANDA YAJA TANZANIA KUJIFUNZA USIMAMIZI WA HUDUMA ZA MAWASILIANO

Image
  Na Mwandishi Wetu TANZANIA imeihakikishia Uganda kuwa itaendelea kuipa ushirikiano katika kujenga uwezo wa usimamizi wa sekta ya Mawasiliano na TEHAMA, sambamba na kudumisha ushirikiano wa kitaalam katika usimamizi wa sekta hizo. Akizungumza wakati alipoukaribisha ujumbe wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) ukiongozwa na Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey uliofika katika Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ziara ya Mafunzo na kubadilishana ujuzi, Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrew Mathew alibainisha kuwa, Tanzania imefanikiwa kusimamia vilivyo sekta ya Mawasiliano kwa kuweka Sera Madhubuti za usimamizi wa huduma za Mawasiliano, huku akiwahakikishia wageni fursa tele ya kujifunza katika sekta ya Mawasiliano. “Tanzania imepitisha sera zinazounga mkono ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano - TEHAMA na mfumo wa kisheria na udhibiti unaounga mkono ukuzaji wa uchumi wa kidijiti,” alisisiti

UFUNGAJI MAFUNZO YA UONGOZI YA WAKAGUZI WASAIDIZI UHAMIAJI

Image
  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mhandisi Hamad Masauni, amefunga  Mafunzo ya uongozi ya wakaguzi wasaidizi wa Uhamiaji katika chuo cha Uhamiaji cha Raphael Kubaga wilaya ya Mkinga, Mkoani Tanga, mwishoni mwa wiki iliyopita. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Uhamiaji wakiongozwa na  Kamishna  Jenerali  Dkt. Anna Makakala. (Picha na Uhamiaji)

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO NOVEMBA 30, 2022

Image