Posts

JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM, KWENDA NA VIPAUMBELE NANE, BAJETI YA 2022/23: WAZIRI DKT.GWAJIMA

Image
   Na MJJWM, DA ES SALAAM     Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima, amesema katika Bajeti ya 2022/23, Wizara yake inatazamiwa kwenda na Vipaumbele 8 vitakavyotumia Jumla ya Bil. 43.3 iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Juni. 30. 2022 jijini Dodoma. Dkt. Gwajima ametoa ufafanuzi huo Julai, 30, 2022 wakati akizungumza na Waandishi wa vyombo mbali mbali vya Habari. Waziri Dkt. Gwajima amevitaja vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na kuratibu afua za kukuza usawa wa kijinsia, uwezeshaji wanawake kiuchumi na kiuongozi na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, watoto na wazee. Kukuza ari ya jamii kushiriki katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo iliyoibuliwa ngazi ya jamii sambamba na kutambua na kuratibu makundi maalum wakiwemo wafanyabiashara ndogondogo (Machinga) ili kuboresha mazingira ya biashara zao.  Dkt. Gwajima amesema maeneo mengine ya vipaumbele ni pamoja na kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia

Rais Dkt.Mwinyi aongoza Mahafali ya 10 Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC), asisitiza jambo

Image
  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa kuwepo kwa changamoto za kiusalama katika Taifa moja kunaweza kuleta athari kwa maendeleo na ustawi wa mataifa mengine. Mheshimiwa Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo katika Mahafali ya 10 ya Wahitimu wa mwaka 2021/2022 wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) kinachotoa mafunzo ya Usalama na Stratejia,hafla iliyofanyika Kunduchi jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa, mfano mzuri ni hivi sasa ambapo kuna mgogoro baina ya mataifa ya Urusi na Ukrane. Ameongeza kuwa, vita hii imeathiri sana uchumi wa dunia kwa kusababisha pamoja na mambo mengine changamoto ya ongezeko la bei za bidhaa, usalama wa chakula, uhamiaji, uhusiano wa Kimataifa pamoja na kutetereka kwa hali ya kisiasa nje ya mataifa hayo. Ameeleza kuwa, katika kukabiliana vizuri na changamoto zinazoikabili dunia hivi sasa, itategemea sana namna Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilivyojitayarisha kukabiliana na hali hiyo pamoja na uhusiano na m

WAZIRI NDALICHAKO AWATAKA WAMILIKI WA VIWANDA KUTOA MIKATABA YA KAZI KWA WAFANYAKAZI

Image
  Na: Mwandishi Wetu   -  MWANZA   Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amewataka wamiliki wa viwanda nchini kutekeleza ipasavyo sheria za kazi ikiwemo kuwapa mikataba ya kazi wafanyakazi wanaowaajiri ili kuepukana na migogoro mahali pa kazi. Akiongea baada ya kufanya ziara ya kukagua utekelezaji wa sheria za kazi na Waajiri katika maeneo ya kazi ya viwandani jijini Mwanza, Waziri Ndalichako amefafanua kuwa suala kubwa alilobaini katika ziara hiyo kuwa wapo wafanyakazi ambao hawana mikataba kabisa ya kazi aidha ya kudumu au ya muda mfupi. “Wafanyakazi wengine wameajiriwa kwa zaidi ya miaka kumi na tano lakini wanakuwa wanapewa mkataba wa mwezi mmoja mmoja, sheria za mikataba ya wafanyakazi zinaweka wazi juu ya aina ya kazi ambazo mfanyakazi anaweza kupewa mkataba wa kudumu au wa muda mfupi, Mikataba mingine huandaliwa tu kwa ajili ya kutuonesha watendaji wa serikali lakini wafanyakazi hawana nakala hizo na hata wakati w

WAZIRI JENISTA AIASA TUME YA UTUMISHI WA UMMA KUSIMAMIA HAKI WAKATI WA KUTOA MAAMUZI YA MASHAURI YA KINIDHAMU

Image
  Na Veronica Mwafisi, Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama ameiasa Tume ya Utumishi wa Umma kusimamia haki wakati wa kutoa maamuzi ya mashauri ya kinidhamu ya watumishi wa umma yaliyowasilishwa ili kutolewa maamuzi. Mhe. Jenista ametoa nasaha hizo jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, kilichofanyika ofisini kwake kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji katika Tume ya Utumishi wa Umma. Mhe. Jenista ameitaka Tume ya Utumishi wa Umma kutoa maamuzi ya mashauri yote ya kinidhamu kwa kuzingatia haki, kwa mujibu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma iliyopo. Waziri Jenista ameongeza kuwa, Tume isipo yashughulikia mashauri ya kinidhamu kwa haki na wakati, inakwamisha maendeleo ya nchi yasipatikane kwa wakati na ndio maana Serikali imekuwa ikiihimiza Tume ya Utumishi wa Umma kutekeleza wajibu wao kwa wakati na kwa kutenda haki. “Jambo la msingi hakikishe

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI AFANYA ZIARA YA KIKAZI MAKAO MAKUU YA TAWA

Image
  NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja (Mb) leo Julai 29, 2022 ametembelea ofisi za Makao Makuu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) zilizopo mkoani Morogoro. Ziara hiyo imelenga kuzungumza na menejimenti na watumishi wa TAWA kuhusu masuala mbalimbali yanayoihusu Mamlaka, ikiwa ni muendelezo wa ziara zake katika Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Masanja ameipongeza TAWA kwa kazi nzuri ya usimamizi wa rasilimali za wanyamapori nchini, licha ya kuwa ni Taasisi changa kuliko zote zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. "Pamoja na uchanga na uchache wenu kwenye Wizara mmeweza kushikamana vizuri , mmepokea majukumu yenu na mnafanya kazi nzuri usiku na mchana", amesema. Sambamba na hilo, Mhe. Masanja amesisitiza nidhamu na uadilifu kwa watumishi wote na kuwataka wahifadhi kuzifuata na kuziishi kanuni za Jeshi la Uhifadhi. "Tufanye kazi kwa uadilifu tukiziangalia kanuni zetu

TANZANIA, URUSI KUONGEZA MAENEO YA USHIRIKIANO

Image
  SERIKALI ya Tanzania na Urusi zimekubaliana kuongeza maeneo ya ushirikiano katika sekta za biashara na uwekezaji,utalii pamoja na utamaduni. . Makubaliano hayo yamefikiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Levonovish Avetsyan katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Balozi Mbarouk amesema kuwa Tanzania na Urusi zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu wa kihistoria ambao uliasisiwa na Waasisi wa Mataifa hayo mawili…….“ kutokana na uhusiano mzuri tulionao umechangia kuimarisha sekta ya utalii, elimu pamoja na afya,” alisema Balozi Mbarouk Balozi Mbarouk aliongeza kuwa Tanzania na Urusi zitaendelea kujikita zaidi kufungua maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii na masuala mengine ya kiuchumi kwa maslahi mapana ya mataifa hayo. Kwa upande wake Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Levonovish Avetsyan ameishukuru Tanzania kw

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI JULAI 30, 2022

Image
 

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA KATIBU MKUU WA ACT-WAZALENDO

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Julai 29, 2022 amezungumza na Katibu Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Ado Shaibu, Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Dar es salaam.  

MAJALIWA: TUNATHAMINI MCHANGO UNAOTOLEWA NA WAHANDISI WANAWAKE

Image
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan inatambua mchango mkubwa unaotolewa na wahandisi wanawake na kwamba inathamini kazi za kihandisi wanazozifanya katika kuchangia ukuaji wa uchumi nchini. “Serikali inatambua umuhimu wa tasnia ya uhandisi kwa ustawi wa nchi nzima, hivyo inahitaji kuhamasishwa na kupewa kipaumbele ikiwa ni pamoja na kutengeneza viongozi wengi zaidi wanawake katika tasnia ya uhandisi. Mheshimiwa Rais amekuwa kielelezo cha ubora, maono, uthabiti na uthubutu kwa viongozi wanawake.” “Kupitia uongozi wake tumeshuhudia namna anavyoifungua nchi yetu ikiwa ni pamoja na kufungua njia kwa wanawake wengi kuwa na uthubutu na kujiamini. Sasa njia iko wazi kwenu, kazaneni na wekeni bidii ili kazi yenu iendelee kuonekana na Taifa lisonge mbele.” Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Ijumaa Julai 29, 2022) wakati akizindua Kongamano la Saba la Wahandisi Wanawake katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA JULAI 29, 2022

Image