Posts

BASHUNGWA ATAKA MICHEZO YA WENYE ULEMAVU KUWA MICHEZO YA KIPAUMBELE

Image
  Na. John Mapepele, WUSM Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent Bashungwa amewaagiza Watendaji Wote, wa Sekta ya michezo kuhakikisha michezo ya wenye ulemavu, hususan soka kuwa miongoni mwa  michezo ya kipaumbele na kuitaka kuingizwa kwenye mifumo rasmi, ya kukuza vipaji, kama UMITASHUMTA na UMISSETA. Mhe. Bashungwa ameyasema hayo leo Novemba 27, 2021 wakati alipokuwa akifungua mashindano ya Afrika ya Mpira wa Miguu kwa watu Wenye ulemavu kwa wanaume (CANAF 2021) katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. “Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambua thamani na fursa zilizopo katika michezo yote, ikiwemo kundi la watu wenye ulemavu. Kwa msingi huo tumechukua jukumu hili, ili kuhakikisha fursa hii inatumika vema kuiweka timu yetu ya soka ya Taifa kwa walemavu, ya Tembo katika ramani ya mchezo huu kimataifa”. Amefafanua Mhe Bashunga Akimkaribisha kufungua mashindano hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya U

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI NOVEMBA 28, 2021

Image
 

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI NOVEMBA 27, 2021

Image
 

WAZIRI WA KILIMO PROFESA ADOLF MKENDA ATEMBELEA SHAMBA LA MICHIKICHI NCHINI UGANDA

Image
  Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda alipotembelea kitalu cha kuoteshea miche ya michikichi katika shamba la Oil Palm Uganda Limited, katika ziara ya kikazi nchini Uganda. Kushoto ni Mkurugenzi wa maendeleo ya mazao wizara ya kilimo, Bw. Nyasebwa Chimagu, Baadhi ya wafanyakazi wakipanda miche kwenye shamba la michikichi katika shamba la Oil Palm Uganda Limited nchini Uganda ambako Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda alitembelea jana. Miche iliyooteshwa katika shamba la Oil Palm Uganda Limited nchini Uganda. Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda akiangalia mbegu za mchikichi alipotembelea kitalu cha kuoteshea miche ya michikichi katika shamba la Oil Palm Uganda Limited, katika ziara ya kikazi nchini Uganda. Kushoto ni Mkurugenzi wa maendeleo ya mazao wizara ya kilimo, Bw. Nyasebwa Chimagu, .................................................. Na Mwandishi Wetu, KAMPALA Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf Mkenda, amezuru kikazi Uganda na kufanya mazungumzo na Waziri wa Kilimo, Mifug

RAIS SAMIA AZUNGUMZA NA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA MAENDELEO LA USWIW

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Uswisi ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Bi. Patricia Danzi kushoto, wakati ujumbe huo ulipofika Jijini Dodoma leo tarehe 26 Novemba, 2021. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Ujumbe kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Uswisi ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Bi. Patricia Danzi, wakati ujumbe huo ulipofika Jijini Dodoma leo tarehe 26 Novemba, 2021.  

RAIS SAMIA AHUTUBIA MKUTANO WA 20 WA TAASISI ZA FEDHA NCHINI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Mkutano wa 20 wa Taasisi za Fedha Nchini wenye lengo la kupitia na kutatua changamoto mbalimbali katika sekta hiyo. Mkutano huo umefunguliwa leo tarehe 25 Novemba 2021 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.