Posts

ZIARA YA RAIS SAMIA SOKO KUU LA KARIAKOO, DAR ES SALAAM

Image
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan afanya ziara ya Kushtukiza katika Soko Kuu la Kariakoo Jijini Dar es Salaam Juni 1, 2021.(Picha na Ikulu).  

MAJALIWA: TUMIENI NISHATI MBADALA

Image
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameziagiza Wizara, Taasisi, Mashirika yote ya Serikali na Sekta Binafsi pamoja na vikundi vya uzalishaji zinazotumia nishati ya kuni na mkaa zianze kutumia nishati mbadala kwa  kupikia na shughuli nyingine za uzalishaji. Ametoa wito huo leo (Jumanne Juni Mosi, 2021) wakati akitoa tamko kuhusu Wiki ya Mazingira Duniani, katika ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma. Amesema kuwa taasisi kama shule, vyuo, hospitali na majengo makubwa  zinapaswa kuzingatia ufungaji wa mifumo ya nishati ya gesi kwa ajili ya kupikia. “Kila Wizara ifanye ufuatiliaji kwenye taasisi zake na nipatiwe taarifa ya hali ya utekelezaji kila baada ya miezi sita inayoonesha ni taasisi ngapi zimefikiwa, zimebadili mifumo au zimejenga majengo kwa kuzingatia hitaji la nishati mbadala” “Suala la uhifadhi, utunzaji, usimamizi na usafi wa mazingira lisiwe jambo linalofanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani pekee, bali tujenge tabia ya kuliona kwamba ni suala la kila siku” amesisitiza

WABUNGE WASHAURI SOMO LA SAYANSI KIMU KUREJESHWA SHULENI

Image
Shirika lisilo la Kiserikali la Agri Thamani Neema Lugangira ambaye pia ni MBUNGE wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo WABUNGE wameishauri Serikali kurudisha mashuleni somo la sayansi kimu ili watoto wafundishwe kuandaa lishe bora tangu wakiwa watoto, jambo ambalo litasaidia kupambana na athari zitokanazo na lishe duni. Akizungumza katika semina lishe kwa Umoja wa Wabunge Wanawake (TWPG), iliyoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Agri Thamani, Mbunge wa Urambo (CCM) Magareth Sitta alisema zamani watoto walifundishwa juu ya kutayarisha chakula lakini hivi sasa hawajifunzi tena. “Serikali kwanini wameondoa somo la domestic sience (sayansi kimu) sisi wengine tulijifunza kule namna ya kuandaa chakula. Na kwanini wanafunzi hawana mashamba ya shule,”alisema. Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Anna Lupembe aliunga mkono kauli ya Sitta ambaye alitaka wataalam wa lishe kutembea katika halmashauri kwa ajili ya kutoa elimu y

WIZARA ZA KISEKTA ZAKUTANA NA WAZIRI WA FEDHA KUJADILI BAJETI KUU YA SERIKALI

Image
Na, Josephine Majura, WFM, Dodoma Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya Mawaziri wa Sekta mbalimbali na kuwahakikishia kuwa maeneo yote ya kipaumbele yatazingatiwa ili kuchochea maendeleo ya nchi kupitia miradi itakayotekelezwa na Wizara hizo. Dkt. Nchemba alisema kuwa lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadili na kupitia maeneo ya vipaumbele kwenye kila sekta ili kuona kama yamejumuishwa kwenye hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kabla ya kusomwa Bungeni Jijini Dodoma Juni 10 mwaka huu. “Nimekutana na viongozi mbalimbali ili kupunguza mazingira yaliyokuwa yakijitokeza nyuma kwamba maeneo ya vipaumbele vya Sekta fulani hayajawekwa sawa”, Alisema Dkt. Nchemba. Aliongeza kuwa maeneo mengi ya vipaumbele yamekuwa yakiwekwa tofauti na matakwa ya Wizara na Sekta husika hivyo kikao hicho kilikaa ili kubainisha maeneo ya vipaumbele ambayo hayakujumuishwa kwenye Bajeti Kuu na kuangalia uwezekano wa kuyajumuisha kama ilivyopen

KAMATI YA BUNGE YATOA WITO WAKANDARASI WABOVU MIRADI YA REA WASIPEWE TENA KAZI

Image
 Veronica Simba na Zuena Msuya. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imetoa wito kwa Serikali kuwa wakandarasi ambao hawakutekeleza miradi ya umeme vijijini kwa kiwango kinachoridhisha katika awamu zilizopita, wasipewe tena kazi hiyo. Wito huo ulitolewa jana, Mei 31, 2021 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dustan Kitandula alipokuwa akitoa majumuisho ya hoja mbalimbali zilizotolewa na baadhi ya Wajumbe, katika semina iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati, ikilenga kuijengea Kamati hiyo uelewa wa kazi zinazoendelea kutekelezwa na sekta husika. Alisema, baadhi ya wakandarasi wamekuwa wakikwamisha jitihada na dhamira njema ya serikali inayolenga kuwafikishia umeme wananchi wote walioko vijijini, kutokana na kuchelewesha kukamilisha miradi hiyo na wengine kutekeleza chini ya kiwango kinyume na mikataba yao. Aliutaka Uongozi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake, hususan Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kutoa kipaumbele kwa wakandarasi

KAMISHENI MNAZOZISIMAMIA NI NYETI KATIKA JESHI LA POLISI: IGP SIRRO

Image
MKUU wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro, akiwavalisha cheo cha Ukamishna wa Jeshi la Polisi (CP) Camilius Wambura (pichani juu) na Hamad Khamis Hamad(Picha ya chini)kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam Mei 31, 2021. Rais Samia aliwateua Kamishna Wambura kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) huku Kamisha Hamad yeye akiteuluwa KUWA MKUU wa Logistic na Fedha. KATIKA ujumbe wake mara baada ya kuwapandisha vyeo, IGP Sirro aliwakumbusha matamanio ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Samia ya kwamba ni kuona Utendaji kazi uliotukuka. "Katika Jeshi la Polisi Kamisheni hizi ni nueti sana, nakufahamu Kamishna Wambura wewe ni mzoefu katika Upelelezi sasa nenda kafanyie kazi mlundikano wa kesi uliopo, Hali kadhalika kwa Kamishna Hamad ninauhakika nafasi uliyopewa utaitekeleza kwa weledi wa Hali ya juu." Alisema IGP Sirro.(Picha na Jeshi la Polisi).  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE JUNI 1, 2021

Image