KAMISHENI MNAZOZISIMAMIA NI NYETI KATIKA JESHI LA POLISI: IGP SIRRO

MKUU wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro, akiwavalisha cheo cha Ukamishna wa Jeshi la Polisi (CP) Camilius Wambura (pichani juu) na Hamad Khamis Hamad(Picha ya chini)kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam Mei 31, 2021. Rais Samia aliwateua Kamishna Wambura kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) huku Kamisha Hamad yeye akiteuluwa KUWA MKUU wa Logistic na Fedha. KATIKA ujumbe wake mara baada ya kuwapandisha vyeo, IGP Sirro aliwakumbusha matamanio ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Samia ya kwamba ni kuona Utendaji kazi uliotukuka.

"Katika Jeshi la Polisi Kamisheni hizi ni nueti sana, nakufahamu Kamishna Wambura wewe ni mzoefu katika Upelelezi sasa nenda kafanyie kazi mlundikano wa kesi uliopo, Hali kadhalika kwa Kamishna Hamad ninauhakika nafasi uliyopewa utaitekeleza kwa weledi wa Hali ya juu." Alisema IGP Sirro.(Picha na Jeshi la Polisi).




 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"