Posts

RAIS SAMIA AHUTUBIA WAFANYAKAZI KILELE CHA MEI MOSI JIJINI MWANZA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Wafanyakazi mbalimbali katika Kilele cha Sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi Kitaifa ambazo zimefanyika Jijini Mwanza leo tarehe 01 Mei, 2021 katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza  

WAFANYAKAZI TANESCO WASHIRIKI MAANDAMANO YA MEI MOSI KITAIFA JIJINI MWANZA

Image
WAFANYAKAZI wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO wameungana na  Wafanyakazi wenzao kutoka Sekta ya Umma na Binafsi katika maandamano ya siku ya Wafanyakazi Duniani maarufu Mei Mosi kitaifa jijini Mwanza Mei 1, 2021. Msafara wa maandamano hayo ulipokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Samia Suluhu Hassan katika uwanja wa CCM Kirumba jijini mwanza ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maslahi Bora, Mishahara Juu, Kazi Iendelee”. Maandamano hayo ya wafanyakazi yalifuatiwa na misafara ya magari ya taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi yakionyesha kazi zinazotekelezwa na taasisi hizo. Rais Samia anatarajiwa kuwahutubia wafanyakazi katika sherehe hizo ambazo ni za kwanza kuhutubiwa na kiongozi huyo wa Serikali ya Awamu ya Sita. Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO, wakijumuika na wafanyakazi wengine katika maandamano ya sherehe za MEI MOSI Kitaifa jijini Mwanza leo asubuhi.  

MANISPAA YA SHINYANGA KUANZISHA MASHINDANO YA USAFI WA MAZINGIRA

Image
    Mkuu wa idara ya Usafi na Mazingira Manispaa ya Shinyanga Kuchibanda Snatus, akisoma taarifa ya mpango wa kuanzisha mashindano ya usafi wa mazingira kwenye Baraza la Madiwani kwa niaba ya Mkurugenzi. Picha zote na Marco Maduhu

SERIKALI IMEFUNGA MTAMBO WA KISASA JKCI WENYE UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI NA MATIBABU YA MOYO (CATHETERIZATION LABORATORY - CATHLAB)

Image
Wataalamu wabobezi wa moyo na wazibuaji wa mishipa ya damu ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimzibua mgonjwa mishipa miwili ya damu ya moyo ambayo ilikuwa imeziba na kushindwa kupitisha damu vizuri. Uzibuaji huo umefanyika kwa kutumia mtambo mpya wa kisasa wa (Catheterization Laboratory - Cathlab) uliounganishwa na mtambo wa  Carto 3 System 3D &  mapping electrophysiology System wenye uwezo wa kufanya uchunguzi, kufunga vifaa visaidizi vya moyo, kuzibua mishipa ya damu ya moyo  na  kutibu hitilafu ya mfumo wa umeme  wa moyo.( Picha na JKCI) Wataalamu wabobezi wa moyo na wazibuaji wa mishipa ya damu ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete  (JKCI) wakimzibua mgonjwa mishipa miwili ya damu ya moyo ambayo ilikuwa imeziba na kushindwa kupitisha damu vizuri. Uzibuaji huo umefanyika kwa kutumia mtambo mpya wa kisasa wa  (Catheterization Laboratory - Cathlab) uliounganishwa  na mtambo wa  Carto 3 System 3D &  mapping electrophysiology System  ambao Serikali umeunu

BOT GOVERNOR LAUDS STAMICO FOR GOLD REFINERY

Image
Bank of Tanzania Governor Prof. Florens Luoga (pictured above) has commended the State Mining Corporation (Stamico) for enabling Tanzania to start gold refining to international standards. He said this after visiting the gold refinery, Mwanza Precious Minerals Limited in Mwanza city on Friday, where he witnessed the developments of the plant including trial production which started on April 21, 2021. “This is miners, gold dealers as well as other stakeholders in the sector. The envisaged dream for Tanzania to stop exporting raw gold is certainly coming to pass”, Prof. Luoga said. The BoT Governor expressed delight to hear that the refinery is capable of extracting other valuable minerals from the gold concentrates. “Given the production capacity of this plant, I believe that it will be able to refine all locally mined gold as well as those from neighbouring countries. These will bear the originality mark from Tanzania, and hence promote Tanzania overseas,” the Governor said.

GAVANA LUOGA AIPONGEZA STAMICO KUANZA KUCHAKATA DHAHABU

Image
  Benki Kuu ya Tanzania imelipongeza Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kwa hatua iliyofikia ya kuanza usafishaji wa dhahabu hapa nchini kwa ubora wa kimataifa. Pongezi hizo zimetolewa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, (pichani juu)wakati alipotembelea kiwanda cha kusafisha dhahabu cha Mwanza Precious Minerals Limited, kilichopo jijini Mwanza Ijumaa na kujionea maendeleo yaliyofikiwa hadi sasa, ikiwemo kuanza uzalishaji. “Haya ni mapinduzi makubwa katika sekta ya madini na ukombozi kwa wachimbaji, wafanyabiashara na wadau wengine wa sekta hii. Ndoto ya Tanzania kuacha kusafirisha dhahabu ghafi naona inaelekea kutimia”, alisema Gavana Luoga. Aidha, Prof. Luoga alivutiwa na taarifa kwamba kiwanda hicho ambacho kinamilikiwa kwa ubia kati ya serikali kupitia STAMICO na wawekezaji wa nje, pia kina uwezo wa kutenganisha dhahabu na madini mengine ambayo yana thamani katika masoko ya madini duniani. “Kwa uwezo wa kiwanda hiki, nina imani mtaweza kununua dhahabu

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI MEI 1, 2021

Image