WAFANYAKAZI TANESCO WASHIRIKI MAANDAMANO YA MEI MOSI KITAIFA JIJINI MWANZA
WAFANYAKAZI wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO
wameungana na Wafanyakazi wenzao kutoka Sekta
ya Umma na Binafsi katika maandamano ya siku ya Wafanyakazi Duniani maarufu Mei
Mosi kitaifa jijini Mwanza Mei 1, 2021.
Msafara wa maandamano hayo ulipokelewa na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Samia Suluhu Hassan katika uwanja wa
CCM Kirumba jijini mwanza ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maslahi Bora,
Mishahara Juu, Kazi Iendelee”.
Maandamano hayo ya wafanyakazi yalifuatiwa na
misafara ya magari ya taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi yakionyesha kazi
zinazotekelezwa na taasisi hizo.
Rais Samia anatarajiwa kuwahutubia wafanyakazi
katika sherehe hizo ambazo ni za kwanza kuhutubiwa na kiongozi huyo wa Serikali
ya Awamu ya Sita.
Comments
Post a Comment