KANISA HALISI LAMUOMBEA MAKUBWA RAIS SAMIA, LAMKABIDHI MUNGU BABA KAZI ALIZOFANYA HAYATI DK. MAGUFULI AMKABIDHI RAIS HUYO KUZIENDELEZA
Baba Halisi wa Uzao akiendesha Sala Maalum ya Kulivusha Taifa la Tanzania, iliyofanyika jana kwenye Viwanja vya Mwanga Community Centre, Mwanga mkoani Kigoma . Na Bashir Nkoromo, CCM Blog Kanisa Halisi la Mungu Baba la Tegeta jijini Dar es Salaam, limefanya Ibada ya 'Kulivusha Taifa', ambapo limemuomba Mungu Baba kumuinua Rais Samia Suluhu Hassan na kumpa ulinzi wake dhidi ya wabaya, afya njema na hekima ya ajabu ili aweze kutenda vema kazi yake ya kuliongoza Taifa la Tanzania. Pia katika ibada hiyo, Kanisa Halisi la Mungu Baba limemkabidhi Mungu Baba kazi zote alizofanya aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dk. John Magufuli, azichukue na kuzikabidhi yeye mwenyewe Mungu kwa baraka zote kwa Rais Samia Suluhu Hassan ili kuziendeleza. Hayo yamejiri katika Ibada hiyo Maalum ya 'Kulivusha Taifa' iliyofanyika kuanzia saa nane mchana hadi saa kumi jioni ikiongozwa na Kiongozi wa Kanisa hilo Baba Halisi wa Uzao, kwenye Viwanja vya Mwanga Community Centre, Mwanga mkoani Kigoma