Posts

WADAU WA NYAMA WENYE MABUCHA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO YA VIFAA VYA KISASA VYA KWENYE MABUCHA

Image
  Kaimu Msajili Bodi ya Nyama Tanzania huyo aliyevaa (koti la suti)  Imani Sichalwe  akiwa na viongozi wa wadau wa Nyama Arusha,viongozi wa kampuni ya watertras na viongozi wa Amana benki.  Kaimu Msajili Bodi ya Nyama Tanzania huyo aliyevaa (koti la suti)  Imani Sichalwe akikagua moja ya mashine za kisasa za kukatia nyama  vitakavyosambazwa na Kampuni ya watertras   Na Vero Ignatus.   Wadau wa Nyama Nchini watakiwa kujiunga Kwenye vikundi na visajiliwe kwa mujibu wa sheria ,Jambo litakalowawezesha kuwa na Vigezo vya kukopesheka kwenye Taasisi mbali mbali za kifedha Nchini. Hayo yamesemwa na Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Nchini Tanzania Imani Sichalwe  ,mara baada ya kumalizika kikao kazi kilichofanyika mkoani Arusha kikihusisha viongozi wa Amana bank, viongozi wa wauzaji nyama Arusha, viongozi wa kampuni ya watertrans  Lengo likiwa ni kujadili na kukubaliana kwa pamoja ni namna gani wauzaji nyama Kwenye mabucha wanaweza kukopesheka.   Sichalwe amesema ni muda mrefu wadau wa nyama ,wa

SINGIDA YATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI BIASHARA USAFIRISHAJI BINADAMU

Image
  Katibu wa Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu, Seperatus Fella, akiweka mkakati wa namna bora ya kukabiliana na biashara hiyo, alipokutana na wadau mbalimbali kwenye mafunzo maalumu mkoani Singida juzi. Afisa wa Sekretarieti hiyo, Ahmad Said Mwen-dadi, akitoa mada kwenye mafunzo hayo. wa Sekretarieti hiyo, Alex Lupilya akitoa mada kwenye mafunzo hayo. Picha ya Pamoja ya baadhi ya wadau walioshiriki mafunzo hayo.   Na Godwin Myovela, Singida WAKAZI mkoani hapa wametakiwa kuwa makini kabla ya kuwaruhusu mabinti kuchukuliwa na kupelekwa maeneo mbalimbali nchini kwa kigezo cha kutafutiwa au kufanya kazi za ndani, badala yake wahakikishe kwanza wanahusisha uongozi wa Serikali ya Mtaa husika ili mchakato huo ufanyike kihalali. Pia ‘dalali’ au mtu yeyote anayetaka kumchukua binti yako hakikisha anakuwa na mdhamini wa kuwezesha kurahisisha   mawasiliano ya mara kwa mara, lengo hasa ni kuwa na uhakika wa mazingira ya usalama wa mwanao huko ae

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU OKTOBA 26, 2020

Image
 

RC TELACK AONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU SIKU YA UCHAGUZI

Image
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake. Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack amesema serikali imejipanga vizuri kuhakikisha Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 28,2020 unakuwa salama huku akiwaonya baadhi ya watu wanaopanga kufanya vurugu kuachana na mipango hiyo. Telack ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Shinyanga ameyasema hayo leo Jumamosi Oktoba 24,2020 wakati akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake ambapo pia amewatahadharisha vijana kuepuka kutumiwa na wanasiasa kuharibu amani ya nchi. “Ninawaomba sana wananchi wa mkoa wa Shinyanga wenye sifa ya kupiga kura wajitokeze kwenda kupiga kura Oktoba 28,2020 ili wachague viongozi wale wanaona wanaweza kuendesha nchi yetu. Muda wa kupiga kura utaanza saa moja asubuhi mpaka saa 10 jioni,niwasihi wananchi wawahi kwenye vituo vya kupigia kura ili kuepuka msongamano usio wa lazima. Baada ya kupiga kura wananc

SERIKALI YAGAWA INJINI ZA BOTI KWA VYAMA VYA WAVUVI KANDA YA ZIWA VICTORIA

Image
Na Mbaraka Kambona, Kagera Katika kuhakikisha shughuli za Wavuvi zinaboreshwa ili kukuza kipato chao, Serikali imegawa Injini za Boti nne (4) aina ya Yamaha zenye thamani ya shilingi milioni 35 kwa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi vinne vinavyofanya shughuli zao katika Ukanda wa Ziwa Victoria. Wakati akikabidhi Injini hizo kwa Wavuvi Wilayani Muleba Mkoani Kagera jana, Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid  Tamatamah alisema kuwa ugawaji wa Injini hizo  ni katika kutekeleza moja ya majukumu ya Wizara ya kuhakikisha wanawezesha upatikanaji wa utaalamu, rasilimali fedha na vitendea kazi ili kuwasaidia Wavuvi kuboresha kazi zao na kuendeleza sekta ya uvuvi kwa ujumla. Dkt. Tamatamah alisema kuwa katika kuhakikisha Vyama vya Wavuvi vinawezeshwa,  mwaka wa fedha 2020/ 2021 Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetenga shilingi milioni mia mbili (200,000,000) kwa ajili ya kuviwezesha vyama vya Ushirika vya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe maji. “Rai yangu kwa Vyama hivi vya Ushirika  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI OKTOBA 25, 2020

Image