Posts

WAKAZI 60,000 BABATI KUPATA MAJISAFI NA SALAMA

Image
Jumla ya wakazi 60,000 wa Mji wa Magugu Wilayani Babati Mkoani Manyara wanatarajia kunufaika na huduma ya maji pindi mradi wa maji unaotekelezwa kwa kutumia chanzo cha Mto Kou utakapokamilika. Hayo yameelezwa Septemba 27, 2020 wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga wilayani humo ya kukagua hatua ya utekelezaji wa mradi huo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA), Mhandisi Idd Msuya. Mara baada ya kupokea taarifa na kujionea hali halisi ya hatua iliyofikiwa ya utekelezwaji wa mradi, Mhandisi Sanga aliielekeza BAWASA kufanya mapitio ya mradi kwenye baadhi ya maeneo ili kuongeza tija.  “Hakikisheni mtandao wa maji unaongezeka ili muweze kuwafikia wananchi wengi zaidi lakini pia wananchi waweze kunufaika kwa Saa 24 kila siku,” alielekeza Mhandisi Sanga. Aidha, Katibu Mkuu Sanga aliielekeza BAWASA kuhakikisha mradi huo wa Magugu unakamilika kwa wakati na kwamba jitihada zifanyike ili utekelezwaji wake ufanyike bil

JPM AKIHUTUBIA WANANCHI ENEO LA MPUGUZI, DODOMA AKIWA NJIANI KUELEKEA MKOANI IRINGA

Image
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Mpuguzi katika Jimbo la Dodoma mjini wakati akiwa njiani kuelekea katika mikutano ya Kampeni za CCM mkoani wa Iringa leo tarehe 28 Septemba 2020 Wananchi wa Mpuguzi mkoani Dodoma wakishangilia mara baada ya Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kusimama katika eneo hilo leo tarehe 28 Septemba 2020 wakati akielekea mkoani Iringa. Wananchi wa Mpuguzi mkoani Dodoma wakishangilia mara baada ya Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kusimama katika eneo hilo leo tarehe 28 Septemba 2020 wakati akielekea mkoani Iringa. Wananchi wa Mpuguzi mkoani Dodoma wakishangilia mara baada ya Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kusimama katika eneo hilo leo tarehe 28 Septemba 2020 wakati akielekea mkoani Iringa.  

MFUMO MPYA WA KITANZANIA WA TAARIFA ZA KIUTUMISHI NA MISHAHARA KUDHIBITI UINGIZWAJI WA TAARIFA ZISIZO SAHIHI

Image
James Mwanamyoto, Dodoma Maafisa Utumishi na Maafisa Tawala 108 waliohitimi Mafunzo ya siku 12 ya Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara wametakiwa kukamilisha usahihishaji wa taarifa za watumishi zilizopo kwenye mfumo wa sasa ili ziweze kuingizwa katika mfumo mpya, kwani mfumo mpya hautoruhusu kuingiza taarifa ambazo sio sahihi na zisizokamilika.  Maelekezo hayo yametolewa jana jijini Dodoma na Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Cosmas Ngangaji wakati akifunga mafunzo hayo yaliyokuwa na lengo la kuboresha utendaji kazi na usimamizi wa rasilimaliwatu na mishahara. Bw. Ngangaji amesema, baada ya kukamilika kwa mafunzo haya na kuanza kutumika rasmi kwa mfumo huu mpya, Serikali inatarajia mfumo mpya utatumika kutatua kero za watumishi kwa ufanisi na kwa haraka zaidi ikiwa ni pamoja na kuwaondolea usumbufu wa kufuata huduma Ofisi ya Rais Utumishi.  Bw. Ngangaji ameongeza kuwa, mfumo mpya utaongeza uadilifu kiutendaji kwani umeweze

TARI YATOA MAFUNZO YA UPANDAJI BORA WA ZAO LA KOROSHO MPWAPWA DODOMA

Image
  Mtafiti  kutoka Tari- Naliendele Programu ya Zao la Korosho, Kasiga Ngiha, akitoa mafunzo ya jinsi ya kuandaa shamba, kulipima na upandaji wa zao la korosho kwa Maafisa Ugani na Wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma jana katika shamba la Magereza la wilaya hiyo. Afisa Kilimo kutoka Kata ya Lufu, Pascal Male (kushoto) na wenzake wakijifunza kutoka TARI namna ya kuweka alama wakati wa mafunzo kwa vitendo ya upimaji wa shamba la korosho kabla ya kupandwa zao hilo. Maafisa Ugani na Wakulima wakijifunza kwa vitendo namna ya upimaji wa shamba la korosho kabla ya kupanda. Mkulima kutoka Kata ya Lupeta, Yohana Mkasanga (Aliye chuchumaa akipima shamba kwa kamba katika mafunzo hayo ya vitendo. Kushoto (mwenye kofia) ni Mratibu wa Kitaifa wa Zao la Korosho kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI Naliendele Mtwara, Dkt.Geradina Mzena akiwa kwenye mafunzo hayo. Afisa Kilimo kutoka Wilaya ya Mpwapwa, Kongwa, Malizia Said (kulia), akijifunza kutoka TARI namna ya kuweka alama

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU SEPTEMBA 28, 2020

Image
 

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI SEPTEMBA 27, 2020

Image