Posts

RAIS WA ZAMBIA HAKAINDE HICHILEMA AWASILI KWA SHEREHE ZA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema tayari amewasili nchini kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania ambapo amepokelewa na Waziri wa Madini Mhe.Anthony Mavunde.  

RAIS RUTTO AWASILI NCHINI KWA SHEREHE ZA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Rais wa Jamhuri ya Kenya  Mh. William Samoei Rutto akipokewa na Waziri wa Madini  Mh. Anthony Mavunde wakati alipowasili nchini Tanzania kwa ajili ya kushiriki katika maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar  

LENGO LA SERIKALI NI KUBORESHA MAISHA YA KILA MWANANCHI TARAFA YA NGORONGORO-NCAA

Image
Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema kuwa ina lengo la kuboresha maisha ya wananchi wa tarafa hiyo kwa kuwaelimisha na kuwahamisha wananchi waliojiandikisha kuhama kwa hiyari kwenda Kijiji cha Msomera Handeni Mkoani Tanga na maeneo mengine nchini. Akizungumza na wananchi wa tarafa ya Ngorongoro kwa nyakati tofauti katika zoezi la uelimishaji, uhamaishaji na uandikishaji kaimu meneja wa Uhusiano kwa Umma wa mamlaka hiyo Hamis Dambaya amesema zoezi la kuwaelimisha wananchi hao litaendelea ili kuhakikisha kila mkazi wa tarafa ya Ngorongoro anahama kwa hiyari.  Amewaeleza wananchi hao kwamba serikali haina nia mbaya kwa kuwashawishi kuhama kutoka ndani ya hifadhi kwani inatambua kuwa iwapo wananchi hao watakubali kuhama wataweza kuboresha maisha yao katika maeneo mbalimbali watakayoamua kuelekea sambamba na kulinda usalama wao kutokana na uwepo wa matukio ya wanyama wakali ndani ya hifadhi.  “Mnaishi katika mazingira magumu hasa kutokana na kukosa uhuru wa kuing

TUME YA UCHAGUZI YAFAFANUA KUHUSU TAARIFA ZA VIGEZO VYA KUOMBA KAZI ZA MUDA ZA WATEMDAJI WA VITUO VYA KUBORESHA DAFTARI LA MPIGA KURA

Image
   

ELIMU YA PSSSF KIGANJANI YAWAFIKIA WANACHAMA MAONESHO YA OSHA

Image
  NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), umewakumbusha wanachama wake kuwa, huduma zote zinazohusiana na uanachama wa mwanachama zinapatikana mtandaoni, (PSSSF Kiganjani). Meneja wa PSSSF, Kanda ya Kaskazini, Bi. Vonness Koka, amesema hayo wakati akiongoza timu ya watumishi wa Mfuko huo kupeleka elimu ya matumizi ya PSSSF Kiganjani kwenye mabanda ya maonesho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), kwenye viwanja vya General Tyre jijini Arusha Aprili 25, 2025. “Tumeanzisha mfumo wa PSSSF Kiganjani unaomuwezesha mwanachama kupata taarifa za Michango yake mahali popote alipo bila ya kufika kwenye ofisi zetu, vile vile mfumo unamuwezesha mstaafu kujihakiki akiwa nyumbani kwake, safarini au mahali popote. Tunawakaribisha wanachama wote waliopo Kilimanjaro, Manyara, Tanga, Arusha na wananchi kwa ujumla, kufika kwenye banda letu ili kupata elimu hiyo ya matumizi ya PSSSF Kiganjani.” Amefafanua Bi. Koka. Amesema, kupitia si

KUTOKA MAGAZETINI LEO APRIL 25 , 2024

Image

TASAF YATUMIA RUZUKU YA BILIONI 800 TANZANIA BARA NA VISIWANI KWA AJILI YA WALENGWA WA KAYA MASIKINI

Image
  Mkurugenzi wa Miradi – Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. John Steven. …………………. Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kipindi cha awamu ya pili ya utekelezaji iliyoanza mwaka 2020 umefanikiwa kutoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni 800 Tanzania bara na visiwani na kufanikiwa kuimarisha kiuchumi wa kaya maskini katika kuhakikisha wanapiga hatua katika maendeleo. Akizungumza leo Aprili 24, 2024 katika Maonesho ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano yanayofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Miradi – Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. John Steven, amesema kuwa walengwa wamefanikiwa kuimarika kiuchumi na kuweza kusaidia familia zao ikiwemo kusomesha na kujenga nyumba. Bw. Steven amesema kuwa katika utekelezaji wa majukumu yao kwa sasa wametoa ruzuku shilingi bilioni 17.5 kwa halmashauri mbalimbali Tanzania Bara na Visiwani katika maeneo ya utekelezaji 35, huku maeneo 18 yakiwa katika mchakato wa utekelezaji. “Miongoni mwa majukumu yet