Posts

TANZANIA KUNUFAIKA NA MIRADI YA MPANGO WA MATTEI (TANZANIA TO BENEFIT FROM MATTEI PLAN PROJECTS)

Image
Tanzania imechaguliwa kuwa moja ya nchi nane za Afrika zitakazopewa kipaumbele na Italia kupitia mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan) ambapo kiasi cha  Euro bilioni 5 za awali kimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.\n\nMiradi hiyo ya kipaumbele kupitia Mpango mpya wa Kimkakati wa Mattei (Mattei plan) ipo katika sekta ya nishati, elimu na kilimo.  Taarifa hiyo imetolewa na Rais wa Chama cha Wafanyabiashara wa Italia, Mhandisi Alfredo Cestari alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) pembezoni mwa Mkutano wa Nne wa Wakuu wa Nchi za Afrika na Italia unaendelea Roma, Italia. \n\nMhandisi Cestari alieleza kuwa utekelezaji wa mpango huo utaanza mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika na Italia, ambapo Serikali ya nchi hiyo itafadhili miradi ya kipaumbele kwa nchi nane za awali za Afrika. Hatua hiyo itahusisha pia kugharamia gharama za upembuzi yakinifu ya miradi itakayopendekezwa. \n\nK

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU JANUARI 29, 2024

Image
 

MELI 13 ZINAHUDUMIWA MUDA HUU BANDARI YA DSM JANUARI 28/2024

Image
  *Hizi hapa dondoo 15 muhimu za kuzingatia dhidi ya propaganda hasi kwa bandari ya DSM 1.Magati yote 12 pamoja na maeneo ya kuhudumia shehena za mafuta yanahudumia meli hadi kufikia muda huu wa leo tarehe 28 Januari 2024, tofauti na wapotoshaji wanaoposha kwa makusudi kuwa ni magati mawili (2) tu ndio yanayofanya kazi kati ya magati 12 yaliyopo. 2.Taarifa zinaonesha ukweli halisi watu wakichapa kazi katika magati yote 12 na kuongeza ufanisi. Kwa mfano, Gati namba Sifuri (0) ambalo ni mahsusi kwa kushusha shehena ya magari nalo linahudumia meli MV Yangze 32 ya mizigo mchanganyiko. 3. Idadi na wingi wa meli bandarini unabadilika ukiona leo foleni meli 20 na keshokutwa ukaona meli 20 haina maana ni zilezile maana yake kuna meli zimehudumiwa na nyingine zimekuja kutaka kuhudumiwa. 4. Ni sawa na shuleni mtu anaweza kuhoji mbona kila mwaka shule zinakuwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne. Maana yake ni kuwa kadri wengine wanavyomaliza shule ndivyo wengine wanaanza shule, wa

WANACHAMA WAFURAHISHWA NA HUDUMA YA PSSSF KIGANJANI MOBILE APP

Image
NA KVIS BLOG/KHALFAN SAID, MNAZI MMOJA WANACHAMA wengi wa PSSSF waliotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Wiki ya Sheria kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, wamefurahishwa na huduma ya PSSSF Kiganjani Mobile App. Huduma ya PSSSF Kiganjani Mobile App, inamuwezesha mwanachama kupata taarifa zote zinazohusiana na uanachama wake akiwa mahali popote kupitia simu yake ya kiganjani, Mtaalamu wa Mifumo ya Kompyuta wa Mfuko huo Bw.Gideon Mwashihongo amesema leo Januari 28, 2024, wakati akitoa elimu ya matumizi ya huduma mtandao. Bw. Kizza Sostenes, Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba, Wilaya ya Temeke, ameupongeza Mfuko huo kwa kutoa huduma zake kidijitali. “Nimefaidika sana baada ya kufika hapa, nimeelekezwa jinsi ya kutumia huduma ya PSSSF Kiganjani na nimeijaribu ni huduma nzuri na rahisi kutumia.” Amesema Bw. Sostenes. Mwanachama mwingine Bi. Lightness G. Msuya, yeye amesema huduma ya PSSSF Kiganjani Mobile App, inasaidia kuokoa muda, kwani yeye kama