Posts

NAIBU WAZIRI PINDA AASA WANANCHI KUHUSU MATUMIZI BORA YA ARDHI

Image
Na Munir Shemweta, MLELE Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amewaasa watanzania kuhakikisha wanakuwa na mipango bora ya matumizi ya ardhi kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo kwa kuwa ardhi iliyopo haiongezeki na idadi ya watu inazidi kuongezeka. Mhe. Pinda amesema hayo tarehe 26 Desemba 2023 nyumbani kwake Kibaoni, Halmashauri ya Mpimbwe mkoani Katavi katika hafla maalum ya chakula aliyowaandalia wananchi na viongozi wa jimbo lake kusheherekea Siku Kuu ya Chrismas. Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda, Naibu Waziri huyo wa Ardhi alisema, wakati serikali ikiandaa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, watanzania wanatakiwa kuwa na mpango wa matumizi ya ardhi huku wakielewa changamoto kubwa iliyo mbele yao ni kuwa ardhi haiongezeki.   ‘’Miaka 25 inayokuja lazima tufikirie hizi hekta na ekari tulizopopewa na Mungu ikaitwa Tanzania inatushoje itakapofika

ZAIDI YA MILIONI 60 ZATUMIKA KUTENGENEZA BARABARA ITUNDUMA

Image
  Msimamizi wa miradi ya TASAF katika Kijiji cha Itunduma Wilaya ya Wanging'ombe Mkoani Njombe Shabani Lukelema akizungumza kuhusu matengenezo ya  barabara yao katika kijiji cha Itunduma. Msimamizi wa miradi ya TASAF katika Kijiji cha Itunduma Wilaya ya Wanging'ombe Mkoani Njombe Shabani Lukelema akishiriki pamoja na wanufaika wa TASAF katika matengenezo ya  barabara yao katika kijiji cha Itunduma. Wahariri wa vyombo vya habari pamoja na baadhi ya viongozi wa TASAF mkoani Njombe wakizungumza na wanufaika wa TASAF wanaotengeneza barabara ya kijiji cha Itunduma wakati walipotembelea mradi huo. Mhariri wa EFM na ETV Scholastica Mazula akicheza na akina mama wanufaika wa TASAF waliopata ajira za mda katika mradi wa barabara ya kijiji cha Itunduma mara baada ya kutembelea mradi huio na kuzungumza nao. Muonekano wa Kipande cha barabara iliyotengenezwa na wanufaika hao. ................................ Mradi wa barabara wenye kilometa 4.4 unaounganisha Vijiji viwili vya Itunduma

RPC MALLYA ATEMBELEA KITUO CHA KUTAMBUA NA KUKUZA VIPAJI VYA WATOTO SONGWE

Image
Na Issa Mwadangala. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Theopista Mallya, Disemba 25, 2023 ametembelea kituo cha kutambua na kukuza vipaji vya watoto kiitwacho Mwakitwange Toto Center kilichopo eneo la Isangu wilayani Mbozi ili kuijionea mambo wanayoshiriki watoto hao kituoni hapo. Kamanda Mallya akiwa ameambatana na watoto wawili ambao aliwahi kukutana nao wakati akitoa elimu ya ushirikishwaji jamii kwa makundi mbalimbali, watoto hao ni Samwel Patrick Ndolimana kutoka Shule ya Msingi Juhudi na Ivanka Klif Nzunda kutoka Shule ya Msingi Haloli wote ni wanafunzi wa darasa la Pili katika shule hizo, kitendo hicho kilimpelekea kuwakutanisha watoto hao na watoto wenzao katika tukio hilo ili waweze kufurahia kwa pamoja. Akizungumza na wazazi/walezi pamoja na watoto hao alisema “Ulinzi wa kuwalinda watoto na wanafunzi unaanza na sisi tuwe makini sana kipindi hiki cha mwishoni mwa mwaka kwani watoto wengi upotea na hufanyiwa ukatili hivyo basi mzazi/mlezi unatakiwa

UFUNGUZI NA UWEKAJI WA MAWE YA MSINGI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO KUENDELA KESHO

Image
Na Fauzia Mussa, Maelezo Zanzibar  SHAMRASHAMRA za kutimiza miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar zinaendelea kesho Disemba 27,2023 kwa uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi atazindua uwanja wa Amaani na miundombinu mengine ya michezo katika uwanja huo uliopo Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi. Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Massoud Othman anatarajiwa kufungua Skimu ya Masingini iliyopo Wilaya ya Magharibi “A”, huku Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla kufungua kituo cha mama na mtoto Uzi Wilaya ya kati Unguja. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Mohammed Mussa atafungua tangi la maji safi na salama Unguja Ukuu wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja. Kwa upande wa Pemba Naibu Spika wa Baraza la Wakilishi Mhe. Mgeni Hassan Juma atafungua Soko la samaki na mbogamboga Machomane Wilaya ya Chakechake pam

KUTOKA MAGAZETINI DESEMBA 26, 2023

Image
 

NAIBU WAZIRI PINDA AKIWA JIMBONI KATAVI

Image
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kavuu wilayani Mlele mkoa wa Katavi Mhe Geophrey Pinda akizungumza na baadhi ya wananchi waliomtembelea nyumbani kwake Kibaoni katika jimbo la Kavuu tarehe 25 Disemba 2023 mkoani Katavi. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kavuu wilayani Mlele mkoa wa Katavi Mhe Geophrey Pinda (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mlele Wolfgun Pinda (Katikati) akiwa jimboni kwake tarehe 25 Disemba 2023 mkoani Katavi. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kavuu wilayani Mlele mkoa wa Katavi Mhe Geophrey Pinda (katikati) akizungumza na mmoja wa wananchi wa Kibaoni, Mlele wakati akiwa jimboni kwake tarehe 25 Disemba 2023 mkoani Katavi. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mlele Wolfgun Pinda.   Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kavuu wilayani Mlele mkoa wa Katavi Mhe Geophrey Pin

KUTOKA MAGAZETINI DESEMBA 25, 2025

Image