Posts

RAIS SAMIA AZINDUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO KUELEKEA KWENYE KILELE CHA TAMASHA LA KIZIMKAZI ZANZIBAR

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Kituo cha Afya cha mama na mtoto Kizimkazi Dimbani tarehe 29 Agosti, 2023 mara baada ya kukizindua katika shamrashamra za kuelekea kwenye kilele cha Tamasha la Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi wengine wakati akikata utepe kufungua Chumba cha Kompyuta na ukumbi wa Mtihani wa Skuli ya Sekondari ya Muyuni B kwenye hafla fupi iliyofanyika Mkoa wa Kusini Unguja Zanzibar katika shamrashamra za kuelekea kwenye kilele cha Tamasha la Kizimkazi tarehe 29 Agosti, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati akikagua Madarasa ya Shule ya Msingi Muyuni B mara baada ya ufunguzi katika Mkoa wa Kusini Unguja Zanzibar tarehe 29 Agosti, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua ugawaji wa Gari la OCD Kizimkazi Mkunguni pamoja na Gari la OCD Makund

DKT. YONAZI: GLOBAL FUND YAIMARISHA SEKTA YA AFYA NCHINI

Image
  NA MWANDISHI WETU – DAR ES SALAAM Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ameupongeza na kuushukuru Mfuko wa Dunia (Global Fund) kwa mchango mkubwa unaoutoa katika kuendeleza mapambano dhidi ya magonjwa ya UKIMWI, Malaria na Kifua Kikuu nchini. Ametoa pongezi hizo wakati akifungua mkutano wa Uundwaji wa Miradi ya Mfuko wa Dunia (Global Fund) kwa kipindi cha mwaka 2024- 2026 uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa hoteli ya APC Bunju Dar es Salaam. Mkutano huo ulioudhuriwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha, Wizara ya Afya, Wizara ya Maendeleo ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Sekretarieti ya TNCM, Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Pamoja na Asasi za Kiraia. Akieleza kuhusu mchango wa Mfuko wa Dunia katika sekta ya afya nchini, Dkt. Yonazi alisema kuwa, nchi imeendelea kupiga hatua kwa kuzingatia ufadhali wanaout

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE AGOSTI 29, 2023

Image
   

MAKALA; WCF YATOA ELIMU YA FIDIA KWA WAFANYAKAZI MAONESHO YA MADINI RUANGWA

Image
NA K-VIS BLOG, RUANGWA Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umetumia fursa ya Maonesho ya Madini wilayani Ruangwa mkoani Lindi yaliyofikia kilele Agosti 26, 2023, kukutana na wadau na kutoa elimu ya fidia kwa wafanyakazi. Sekta ya madini ni miongoni mwa maeneo yanayotoa ajira kwa watanzania wengi ambao kwa mujibu wa sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi, mwajiri anapaswa kujisajili na Mfuko na kuwasilisha michango kila mwezi na endapo mfanyakazi ataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi, ni wajibu wa  WCF kumlipa fidia. Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), imeutaja Mkoa wa Lindi kuwa na Madini Mkakati sita ambayo ni Chuma, Kinywe, Dhahabu, Shaba, Magnesite, pamoja na Madini Muhimu manne ambayo ni Jasi, Chokaa, Chumvi na Chuma hali inayoonyesha kuwa ajira nyingi zitokanazo na upatikanaji wa madini hayo zitazalishwa. Aidha afisa Madini Mkazi Mkoa wa Lindi Mhandisi Iddi Msikozi, amesema Maonesho hayo yaliwaleta pamoja wadau wa sekta hiyo kutoka nchi zaidi ya 10 d