Posts

WAZIRI MKUU AALIKA WAWEKEZAJI VIWANDA VYA MBOLEA

Image
 *Ashiriki ufunguzi wa Jukwaa la Uchumi WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaalika wawekezaji waliobobea kwenye sekta ya mbolea ili waje kufungua viwanda vya mbolea nchini. Ametoa mwaliko huo leo (Alhamisi, Julai 27, 2023) wakati akizungumza kwenye mjadala uliohusu Uimarishaji wa Soko la Mbolea kama njia ya kuondoa njaa barani Afrika uliofanyika kwenye kituo cha mikutano na maonesho cha Expo Forum, jijini St. Petersburg, Urusi. Amesema uamuzi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kuongeza bajeti ya kilimo una nia ya kuifanya Tanzania iwe eneo la uzalishaji la kulisha Afrika Mashariki, SADC na bara zima la Afrika. “Bado tuna changamoto ya upatikanaji wa mbolea kwa sababu ikikosekana inaathiri uzalishaji wa chakula.” “Mbolea kwa sasa ndiyo msingi wa uzalishaji chakula. Uzalishaji wetu unatumia zaidi ya asilimia 80 na kwa maana hiyo tunalazimika kutumia fedha nyingi ili kuagiza mbolea kutoka nje na msisitizo wa sasa ni kuzalisha mbolea yetu.” “Tunatumia fursa hii kutafuta marafiki ambao wako ta

TANESCO YAELEZA MAFANIKIO VIPAUMBELE ILIVYOJIWEKEA KUTEKELEZA MWAKA 2022

Image
  NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini TANESCO, Bw. Maharage Chande amesema vipaumbele saba vilivyowekwa na shirika hilo kwa ajili ya utekelezaji mwaka 2022 vimefanikiwa. Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam Julai 27, 2023 kwenye kikao kazi baina ya uongozi wa juu wa shirika hilo, Msajili wa Hazina na Wahariri wa vyombo vya habari. Alivitaja vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na Watu, Wateja, Ufanisi, Miradi ya kimkakati, Kutafuta rasilimali fedha, Mahusiano na kuwashirikisha wadau na Kudhibiti vihatarishi na utawala bora. Akifafanua alisema mambo mengi yaliyofanikiwa katika vipaumbele hivi yamevunja rekodi na hayajawahi kutokea katika historia ya shirika hilo. Alisema kipaumbele cha kwanza walichojiwekea ni watu (wafanyakazi) na kubainisha kuwa eneo hilo ana shauku nalo kwani dunia nzima unapotaka kujua kama umefanikiwa katika eneo hilo unapima kuridhika kwa wafanyakazi (Staff engagement) katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi. “Kwenye

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI JULAI 27, 2023

Image