Posts

WAISLAM SINGIDA WAPONGEZA ZOEZI LA UGAWAJI NYAMA SADAKA YA CHINJA

Image
Na Dotto Mwaibale, Singida WAISLAM Singida wamepongeza utaratibu uliotumika kugawa wanyama waliochinjwa kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Eid Ul Adha ambayo inafanyika leo duniani kote. Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ugawaji wa wayama hao mjini hapa walisema zoezi hilo kwa mwaka huu limeratibiwa vizuri kwani waislam na wananchi wengi wamepata sadaka hiyo tofauti na mwaja ambapo licha ya wanyama hao kuwa wengi kulikuwa na ujanja ujanja uliosababisha wengi wao kukosa. Mkazi Mungumaji katika Manispaa ya Singida, Amina Hamadi alipongeza utaratibu uliofanyika wa ugawaji wa sadaka hiyo kwa kusema mwaka jana hakupata kabisa licha ya kuwepo jirani na kambi ya uchinjaji maeneo ya Karakana. “Mwaka jana nilishinda kutwa nzima nikiwa na wenzangu lakini hatukupata sadaka hii lakini leo tumepata mbuzi mmoja tugawane watu wawili jambo ambalo sikulitegemea kabisa,” alisema Amina. Abubakar Ntandu aliyekuwepo kwenye zoezi hilo alisema utaratibu uliofanywa na Taasisi ya uchinjaji wa wafany

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI JUNI 29, 2023

Image
 

WAZIRI MKUU ATOA AGIZO KWA WATENDAJI WA HALMASHAURI

Image
NA OFISI YA WAZIRI MKUU, DODOMA *Awataka wahakikishe maeneo yote yanayotwaliwa yanalipiwa fidia WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezielekeza halmashauri zote nchini zihakikishe maeneo yote yanayotwaliwa kutoka kwa wananchi yanalipiwa fidia kwa wakati ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza siku za usoni. Amesema kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi kwenye maeneo mbalimbali nchini yakiwemo na ya jiji  la Dodoma ya kutolipwa fidia baada ya maeneo yao kutwaliwa na halmashauri ya jiji. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Juni 28, 2023) wakati akitoa hoja ya kuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mkutano huo umeahirishwa hadi Agosti 29 mwaka huu. Amesema mahitaji ya uendelezaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo kuanzisha makazi yameendelea kuongezeka. “Ongezeko hilo ni muhimu likazingatiwa katika upangaji wa miji yetu hapa nchini.” Pia, Mheshimiwa Majaliwa amezielekeza halmashauri zote kupima maeneo kwa ajili ya shughuli za

MIKATABA YA UENDELEZAJI BANDARI ITAZINGATIA MASLAHI YA NCHI-MAJALIWA

Image
NA OFISI YA WAZIRI MKUU, DODOMA  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha kuwa mikataba ya utekelezaji wa makubaliano ya uendeshaji wa maeneo ya bandari nchini kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya  DP World  itazingatia maslahi ya nchi na kuleta manufaa kwa Taifa letu.   Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Juni 28, 2023) wakati akitoa hoja ya kuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo amesisitiza kuwa makubaliano yaliyoingiwa yanalenga kuweka msingi wa ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai.   Mheshimiwa Majaliwa amesema kwa kuwa bandari ya Dar es salaam ndiyo kitovu cha huduma za bandari nchini Serikali iliamua kutafuta Kampuni yenye uwezo na uzoefu mkubwa katika uendeshaji wa bandari duniani kwa teknolojia za kisasa ili kuiwezesha bandari hiyo kufanya kazi kwa ufanisi, kuongeza mapato ya nchi na kuchagiza sekta nyingine za kiuchumi.   Amesema Serikali za Tanzania na

WAZIRI MKUU MAJALIWA AELEKEZA WAAJIRI KOTE NCHINI KUHAKIKISHA WANALIPA MICHANGO YA WAAJIRIWA PAMOJA NA MALIMBIKIZO YA TOZO KATIKA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII

Image
K-VIS BLOG, DODOMA Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muunganow a Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewaelekeza waajiri kote nchini kutunza kumbukumbu za malipo ya michango ya waajiriwa pamoja na kulipa malimbikizo ya michango ya watumisji na tozo katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ifikapo tarehe 30, Septemba 2023. Waziri Mkuu ameyasema hay oleo wakati akitoa hotruba ya kuliahirisha Bunge jijini Dodoma Juni 28, 2023. Mhe. Majaliwa pia ametoa maelekezo kwa Wizara ya Maji kudhibiti upotevu wa maji wakati wa kusambaza maji kwa wananchi sambamba na kufufua visima vya zamani ambavyo vina maji kwa wingi na havitumiki ili kuwezesha maji kupatikana kwa vipindi vyote vya mwaka. Aidha ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuimarishe uratibu wa mifugo na kuwaelimisha wafugaji kufuga kwa tija na kuwa na idadi ya mifugo inayolingana na uwezo wa maeneo waliyonayo. Hatua hii iende sambamba na kumiliki maeneo na kupanda nyasi kwa ajili ya malisho. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba ya kuliahirisha

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AKUTANA NA UJUMBE WA CBM OFISINI KWAKE

Image
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga na Ujumbe wa Shirika la Kimataifa la Christian Blind Mission (CBM) uliomtembelea Ofisini Kwake Ngome Jijini Dodoma. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza na ujumbe kutoka Shirika la kimataifa la Christian Blind Mission (CBM) uliomtembelea Ofisini kwake Ngome Jijini Dodoma. Mkurugenzi wa Maendeleo Jumuishi (CBM) Bwn. Dominique Schlupkothen akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga ambaye hayupo kwenye picha alipomtembelea Ofisi kwake Ngome Jijini Dodoma. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akitoa zawadi kwa Mkurugenzi wa Maendeleo Jumuishi (CBM) Bwn. Dominique Schlupkothen alipotembelea ofisi kwake Ngome Jijini dodoma. Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Christian Blind Mission (CBM) Nchini Bi. Nesia Mahenge akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya Wazi

TMDA KUENDELEA KUTENGENEZA MAZINGIRA MAZURI KWA WAFANYABIASHARA WA VIFAA TIBA

Image
 Na Emmanuel Massaka wa Michuzi TV MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba(TMDA)imeweka wazi kwamba itaendelea kuwawekea mazingira rafiki kwa wafanyabiashara wa usambazaji, vitendanishi na vifaa tiba kwa lengo kuwawezesha kufanyabiashara hiyo na hatimaye kuinua uchumi kwa ujumla. Akizungumza leo Juni 27, 2023 jijini Dar es Salaam kwenye mkutano uliohusosha wasambazaji na wauzaji wa vifaa tiba, vitendanishi pamoja na dawa Meneja wa TMDA Kanda ya Mashariki Adonis Bitegeko amesisitiza TMDA itahakikisha inaendana na dhamira ya Awamu ya Sita katika kuwainua wafanyabiashara nchini. Amefafanua kwamba TMDA wanatekeleza kwa vitendo dhana ya kuwainua wafanyabiasha hao , hivyo wamekutana na wadau hao kwa ajili ya kujengeana uwezo na kubadilisha mawazo huku akisema kwa kutambua umuhimu wa wadau hao ndio maana hakuna msambazaji wa vifaa tiba waliyemfungia. " TMDA tumejikita katika kutoa elimu ikiwemo kwa watoa huduma na kwetu sisi ni huduma mbele na kuwashawishi wafanyabihashara wafanye kazi kwa w