Posts

CHAMA CHA WASTAAFU WA BENKI KUU YA TANZANIA (BOTRA) WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI, KUPITISHA MPANGO KAZI 2023.

Image
  Mwenyekiti wa Chama Cha Wastaafu wa Benki Kuu ya Tanzania (BOTRA) Bi. Grace Rubambe akifungua mkutanomkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa BoT jijini Dar es Salaam Aprili 27,2023. ................................................... NA JOHN BUKUKU, DAR ES SALAAM. Wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi nchini wametakiwa kuwa na utamaduni wa kujiandaa mapema kustaafu kwa kutengeneza mazingira rafiki ya kiuchumi jambo ambalo litawasaidia kuishi maisha ya heshimu katika jamii kipindi wanapostaafu. Akizungumza lo tarehe 27/4/2023 Jijini Dar es Salaam katika Mkutano Mkuu wa Mwaka, Mwenyekiti wa Chama Cha Wastaafu wa Benki Kuu ya Tanzania (BOTRA) Bi. Grace Rubambe, amesema mkutano mkuu huo umelenga kufanya uchaguzi wa viongozi, kujadili mpango mkakati, Bajeti pamoja na kupitisha mpango kazi wa mwaka 2023. "Tunatarajia katika mkutano huu kuchangua viongozi watakaotuongoza katika kipindi cha miaka mitatu ijayo" amesema Bi. Rubambe. Bi. Rubambe amesema kuwa

KATIBU MKUU HAZINA ATETA NA BALOZI WA DENMARK NCHINI TANZANIA

Image
  Na Joseph Mahumi, WFM, Dar es Salaam Denmark imeahidi kuendeleza ushirikiano zaidi na Tanzania katika jitihada zake za kuimarisha uchumi na maendeleo ya wananchi kwa kutoa fedha na misaada ya kiufundi katika sekta ya mbalimbali ikiwemo afya. Ahadi hiyo imetolewa na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Mette Norgaard Dissingspandet alipokutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu El-Maamary Mwamba, katika Ofisi Ndogo za Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam. “Denmark imekuwa ikishirikiana na Tanzania kwa miaka mingi kwa kusaidia utekelezaji wa bajeti ya Serikali, kusaidia ujenzi wa mifumo ya udhibiti wa matumizi ya fedha za Serikali, kuimarisha mchango wa sekta binafsi katika kukuza uchumi na masuala ya afya kupitia ubia wa sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) kwenye Asasi zisizo za Kiserikali (AZAKI) ambapo ushirikiano huo umeleta matokeo chanya kwenye sekta hiyo” alisema Mhe. Mette Mhe. Mette amepongeza juhudi zinazochukuliwa na serikali

WAFANYAKAZI WA TASAF WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI

Image
  Wafanyakazi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF wametakiwa kufanya kazi kwa ueledi na kuzingatia maadili huku wakiepuka ubaguzi wa aina yoyote katika utekeleaji wa majukumu yao. Hayo yamesemwa leo Alhamisi Aprili 27, 2023 na Katibu Mkuu Ikulu, Mululi Mahendeka alipokuwa akifungua Mkutano wa Mwaka wa wafanyakazi hao unaofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa APC Bunju, Dar es Salaam, Bw Mahendeka amesema kwa moja ya changamoto zinazoukabili mfuko huo ni baadhi ya wanasiasa kupotosha lengo halisi ya Mfuko na kuhusisha kazi zake na itikadi za kisiasa na ukabila. Amesema kwa kuwa wako wanasiasa, kwa malengo wanayoyajua wao, wamekuwa wakieneza habari potofu kuwa kazi wa Mfuko zinahusiana na ikitadi za kisiasa, ni jukumu la wafanyakazi hao kuhakikisha wanafanya kazi kwa kufuata taratibu zilizopo na hivyo kuepuka ubaguzi wa itikadi za kisiasa, kidini na kikabila. “TASAF ni taasisi ya Serikali na hivyo inafuata taratibu za kiserikali. Hakikisheni mnafanya kazi kwa bidi ueledi na maar

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN PAMOJA NA RAIS WA RWANDA MHE. PAUL KAGAME WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023. Rais wa Rwanda Mhe. Kagame amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya Kikazi ya Siku 2. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame wakati wakizungumza na Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Mazungumzo Rasmi na Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuzungumza na Waandishi wa Habari Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023

PSSSF YAPITA "BANDA KWA BANDA" KUWAFIKIA WANACHAMA WAKE KWENYE MAOENSHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI

Image
  NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO. Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na kutoa elimu kwa wanachama na wananchi wanaotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, viwanja vya Tumbaku mjini Morogoro, pia unapita “Banda kwa Banda” ili kuwafikia wanachama wake, Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko huo Bw. Abdul Njaidi amesema. Bw. Njaidi amesema Mfuko unashiriki Maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu na kuwahudumia wanachama wake ambao ni wastaafu lakini pia watumishi wa Umma na Mashirika ambayo Serikali inamiliki hisa asilimia 30. “Lakini tukumbuke kuwa watumishi walio kwenye viwanja hivi nao pia wanawahudumia wananchi kwenye mabanda yao, hivyo tumeona tugawane majukumu, baadhi yetu wako bandani kutoa elimu na huduma kwa watakaofika na sisi tunapita banda kwa banda kuwahudumia." Alifafanua Bw. Njaidi ambaye alifuatana na Afisa Matekelezo Mwadamizi wa Mfuko huo Bw. Charles Mahanga. Akifafanua alise

"NAWASHUKURU WCF KWA KUNIWEZESHA KUYAMUDU MAISHA"-MNUFAIKA WA FIDIA

Image
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO. MNUFAIKA wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Deus Anthony, ameushukuru Mfuko huo kwa kumuwezesha kuyamudu maisha licha ya kupata Ulemavu wa Kudumu uliotokana na Kazi. Mnufaika huyo mkazi wa Morogoro ameyasema hayo leo Aprili 27, 2023 kwenye Maonesho ya Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya mahali pa kazi kwenye viwanja vya Tumbaku mjini humo. “Nilikatika mguu   wa kushoto wakati nikiwa kazini mwaka 2017, WCF wamekuwa na mimi katika matibabu hadi kupona.” Alisema hawakuishia hapo, “Nilipata Ulemavu wa Kudumu, wameninunulia mguu wa bandia naweza kutembea vizuri bila ya shida yoyote,” amefafanua. Bw. Deus ambaye wakati anaumia kazi yake ilikuwa ni udereva amesema pensheni ya kila mwezi anayolipwa na WCF ameweza kudunduliza na kununua bajaji. “Nawashukuru WCF kwa kuniwezesha kuyamudu maisha, hivi sasa nafikiria kukodi shamba ili nilime maaharage huko Mikumi.” Amesema Kuhusu ushiriki wa WCF kwenye Maonesho hayo yanayofanyika Kitaifa

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI APRILI 27, 2023

Image